UKIMUUMIZA MTU KWENYE MAPENZI NAWE JIANDAE KUUMIZWA


Mada yangu ya leo inaweza kuwa kali kwa maana ya ujumbe unavyosomeka kwenye kichwa cha habari; Ukiumiza Katika Mapenzi, Hufi Mpaka na Wewe Uumizwe!
Nimeamua kuandika mada hii kutokana na vilio vingi vya watu walioumizwa na mapenzi. Kusema kweli wengi wanaumizwa sana, hasa siku hizi. Hali ya uaminifu katika mapenzi haiko kama enzi za wazee wetu. Si kama enzi za mzee Anjelus (baba yangu).
NINI MAANA YA KUUMIZWA?
Kuumizwa katika mapenzi si kupigana au kujeruhiana, bali ni kile kitendo cha kuuvuruga uhusiano. Na kitendo hiki kwa kawaida hufanywa na upande mmoja bila ridhaa ya upande wa pili.
Mfano, una mtu wako. Awe mchumba, mke au mpenzi. Mnapendana sana. Na kila siku, kila mmoja anamhakikishia mwenzake kuhusu kudumisha uhusiano wenu.
Sasa ghafla inatokea mmoja anakata uhusiano huku penzi bado motomoto. Hapo si ina maana aliyekatiwa uhusiano lazima ataumia sana?
Au, wawili wanapendana, wanapanga mipango mingi ya mbele kuhusu mapenzi yao kiasi kwamba kila mmoja anaamua kuacha vyote ili kuimarisha penzi. Lakini siku inafika ghafla mmoja anaua uhusiano. Anakuwa hapokei simu, hatumi meseji tofauti na zamani mpaka mwenzake anajua hapa nimeshapigwa chini.

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU,BONYEZA LIKE BUTTON

No comments:

Theme images by pollux. Powered by Blogger.