Chombezo : Dada Emmy (Muuza Ubuyu) Sehemu Ya TISA (9)




Niliduwaa na kubaki nashangaa "jamani mbona mambo haya yananikuta mimi sasa ni harakati gani nazifanya mimi nataka niishi kwa amani lakini mbona huyu elibariki ananifanyia hivi sawa tu mungu atanisaidia tu" niliongea huku machoz yanatoka nikasahau mataa pale yaliruhusu nilichosikia honi nyuma yangu piiiii piiiiiii pooooooo!!!!
Nilikanyaga mafuta nikaanza kuendesha gari huku kichwani bado nina msongo wa mawazo sana, nilitamani sana kumuomba msamaha kaka rafiki maana dhamiri ilikuwa inanihukumu kwa nilivyomwambia ila kabla sijampigia namba ngeni iliingia nikapark gari pembeni.
"Halllo" niliongea baada ya kuweka sikioni
"Yes emmy mzima wewe" nilisikia sauti nene mno ya kunguruma.
"Mimi mzima nani wewe"
" mimi ni kaka rafiki" alijibu
"Mmh kaka rafiki mbona sauti sio yako au unaumwa?? Nilishangazwa na ile sauti.
" nina mafua kidogo upo wapi sasa?? Aliuliza
"Nipo sabasaba maonyesho nilikuwa nadrive nimepaki pembeni"
"Sasa nataka kuonana na wewe leo saa mbili" alizidi kuongea kwa sauti nzito mnoo
"Mmh wapi na mbona mida hiyo ya usiku huwa mimi sitoki"
" hii ni kwa manufaa yako na usalama wako njoo pugu road nitakuelekeza pa kwenda" aliongea na kukata simu.
Nilibaki na mshangao mkubwa nikajiuliza mambo mengi kichwani moja sauti ile haiendani na ya kaka rafiki hata kidogo, pili ongea yake ni ya command/
kuamrisha ni tofauti na kaka rafiki, tatu namba ile iliyonipigia ni namba ambayo niliwahi kuiona mahali si ya kaka rafiki, jingine kubwa zaidi kaka rafiki hataki tuonane iweje huyu kaka rafiki wa leo hatafute tuonane kirahisi namna hiyo na wakati anachofanya mara zote kaka rafiki ni kunipa maelekezo na kukata simu sio kutaka tuonane.
Mambo haya yaliniumiza kichwa nikasema nooo nampigia kaka rafiki mwenyewe kwenye simu nina namba zake sita nikaanza kujaribu ya kwanza haipatikani mpaka ya tano haipatikani nikapata maswali "uenda ni kweli yule kaka rafiki lakini nitamsubiri anipigie kwa mara ya pili"
*********"*****
Nililala mnooo hata sikula japo nilipofika nyumbani nilipika nikawasha tv hapo kuangalia vipindi vya ubuyu matokeo yake usingizi ukanipitia, niliota kitu cha ajabu sana tena juu ya usaliti mkubwa.
ILIVYOKUWA.
nilikuwa nimesimama kutazama bahari nyuma yangu alikuwa mwanaume aliyenishika kiuno alikuwa ni mtu mwenye misuli..
"Vipi baby umepapenda hapa" aliuliza.
"Saana baby nimependa mandhari yake"
"Unajua najaribu kufanyq kila niwezalo hili kukusahaulisha yale matatizo yaliyokukuta"
"Baby kila siku unasema hivyo yalinikuta matatizo naomba nikumbushe kilitokea nini baby"
"Esta mpenzi wangu ni mambo mengi nasubiri hali yako itengamae nitakwambia usijari"
"Mbona hali yako ipo sawa pleasee baby niambie kilitokea nini??
Ilikuwa siku moja nikiwa nimetoka kazini usiku kwasababu ya mambo mengi na kazi iliitajika ndani ya siku tatu mbele ikamilike kutokana muda mdogo ulibaki ilibidi nitumie muda wa ziada kuifanya ile kazi.
Siku hiyo nilitoka kazini usiku wa saa nane ili nipumzike masaa manne kisha nirudi tena ofisini. Nikiwa njiani ghafla nililiona gari mbele yangu likiwa limebeba kitu kama gunia kwenye bonnet niliendelea kutazama ndipo nilipogundua alikuwa furushi tu ila ulikuwa ni mwili wa mtu baada ya kuona mkono mmoja ukining'inia nilizima gari na kuchomoa bastola yangu kiunoni, nilitazama mbele nikasikia wale watu wakisema.
" jamani mume hakikisha amekufa kweli maana kama akipona ushahidi wote utakuwa wazi" aliongea mmoja katu yao.
"Yeah kwa kipigo kile sidhani kama atakuwa hai ila jebu ebu hakikisha" aliongea wa pili
"Jamani heee muda mbya mtupeni baharini huko watu wa patrol watapita muda si mrefu"
Walikimbia wote na nilibaki peke yangu nikasogea mpaka eneo la tukio ndipo nikakuta furushi kuubwa lenye damu nyingi heee kumbe ni mwanamke ikabidi nimchunguze kwa hali ile nilijua amekufa lakini nilisikia akikohoa ndipo hapohapo kwa shida sana nilimbeba kwenye gari nq kufanikiwa kumuingiza ghafla polisi wa patrol wakatokea.
"Halllo unafanya nini hapa usiku huu wewe ni mwalifu" alihoji afande mmoja mweny mwili mpana mno.
"Aaha naomba tuokoe uhai wa binti yupo nyuma nikiwa natoka kazini nilikuta watu watano wakiutupa mwili huu hapa nilishindwa kuwatackle kwasababu walikuwa ni wengi hivyo nikawasubiri walipoondoka nikaenda kutazama ndipo nilipomkuta binti huyu akiwa mahututi mwanzi nilijua amekufa ila baada ya muda akakohoa nikaona nimuwaishw hospitali kwenye kitengo chq dharura naomba msahada wenu" nilioongea huku nafungua mlango wa gari niwaonyeshe jinsi ulivyokuwa.
"Haloo hili jamaa ni liongo naona hawa ndio walee afande ambao ni wauaji wanaowatelekeza wale ambao uwafanyia uhalifu sasa tumekukuta na kithibiti kesi imekamilika"
Nilitetemeka sana nikaanza kujitetea pale ila hawakutaka kunielewa kabisa.
JE NI KIPI KITAENDELEA KATIKA SIMULIZI HIYO YA EMMY.
KUMBUKA HIYO NI NDOTO YAWEZA KUWA KWELI AU NI MAWAZO TU YA EMMY.
ILA NINGEPENDA KUWAKUMBUSHA KUWA SIMULIZI HII IMEJENGWA KWA MFUMO TOFAUTI MAANA MATUKIO AYAENDI KWA KUFATA MPANGILIO ULIOZOELEKA, TUKIO MOJQ ALIISHI LINALUKIWA TUKIO JINGINE YOTE NI KUKUFANYA UPENDE KAZI UANDISHI NA KUZIFATILIA.
YOTE HAYA TUNAYOSOMA NI MATUKIO YA NYUMA EMMY ANAMSIMULA RAFIKI YAKE CINDY, EMMY WA SASA NI MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU KTK UHALISIA HIVYO TUWE MAKINI KUFATILIA HII SIMULIZI.
Suddenly simu yangu ikaita na kutoa kwenye ndoto nilishtuka sana maana tukio lile la ndoton ni zito sana.
"Hello"
"Yeah emmy mzima?
" mzima mamdogo, upo wapi mbona kimya' niliposikia nilitambua ni mama mdogo love.
"Nipo mwanangu hata nashaangaa hu mzima kabisa? Alionyesha mshangao kweli
" yeah ma kuna nini niambie" nilizidi kuhamaki pia
"Noo hakuna nilitaka kujua hali yako kama ni mzima basi nashukuru" alimaliza akakata simu.
Ilinibidi nikae kitako nifikirie nini kimetokea na mamdogo kunipigia simu muda ule ila tokea awali nilianza kuhisi kuna namna ambayo mamdogo love na salma wanashirikian na elibariki ambaye kwa sasa ni kama adui yangu. Akili haikunipa kabisa nikajisemea moyoni "hapa leo silali lazima nijue nini kinaendelea" niliamka japo nilikuwa na uchovu nikanawa uso nikapaka lotion yangu kidogo usoni kwa ule muda (00:23) niliona nivae pensi yangu ya kombati ambazo elikana aliniletea kipindi cha nyuma nikapiga na tshert, simple zangu nikachukua kadi zangu za benki na kiasi kidogo cha pesa nikaweka mfukoni, sikuwa nahitaji gari kwa muda huo, nilidhamiria kukodi bodaboda na kwakuwa kijiweni pale kijichi ccm ni maarufu kwangu haikuwa shida kufikiria nitafika saa ngapi.
Nilifunga geti nikaanza kutembea mwendo kama wa teja yote ilikuwa ni kujiami maana ile mida mibaya hasa kwa mimi mtoto wa kike lolote linaweza kutokea. Sikupiha hatua nyingi simu yangu ikaita nikajivuta kwenye mti nikapokea.
"Mamdogo"
"Yeah emmy umelala? Aliuliza mama
" yeah nimelala upo wapi? Nilimuuliza kwani safari ile ilikuwa ni kwake
"Nipo nyumbani nimelala" mmh nilishtuka kuniambia yupo nyumbani kalala na uku nilisikia sauti za watu wakiongea kwa pembeni yake tena inaonekana wapo bar au sehemu mojawapo ya starehe. Nilikata simu nikijua nitapata vipi.
"Aaha sista emmy"
"Niambie muddy mauwezo"
"Poa sista lake unaruka wapi now dada lake?
" nitaka unirushe temeke mikoroshini now ngapi pale mshizi wangu?
"Shingi saba/elfu saba dada lake"
"Poa nivushe mdau"
Nilijaribu kuongea slang za mtaani ili mradi niweze kuendana na muktadha na kurahisisha maongexi, muddy ni kijana ambaye nafahamiana nae muda sana toka naaminia kijichi na kabla sina gari alikuwa ananipeleka nitakapo kwa bei rahisi, maana hiyo elfu saba kwa mwingine angemwambia kumi na tano hadi elfu ishirini.
****************"""
Nilishangaa kutomkuta mamdogo na wakati aliniambia yupo nyumbani kalala, nilitazama mazingira kwa haraka haraka niligundua kile chumba hakikuwa na mtu kama sio siku tatu ni wiki kabisa kulikuwa na vumbi, shuka lilitandikwa vizuri na midori ililazwa kitandani, nilitumiq simu yangu kutazamia mule ndani. Nilianza kufanya usafi taratibu uku nasikiliza muziki kwenye simu yangu maana chumba chenyewe hakikuwa na umeme.
Nililala baada ya kumaliza kila kitu mpka nikasahau kuzima simu iliimba mpaka asubuhi nilishtuka alarm ilipoita ambao ni muda niliojipangia kuamka kusoma.
Muda uliyoyoma na simu yangu ilizima chaji kabisa nilipokuja kushtuka ilikuwa imetimu saa moja kamili, niliamka nikafanya usafi wa mazingira wakati natoka nikamuona fatuma/mam bakari.
"Shoga mzima wewe? Aliongeaa mama bakari
" mzima vipi kwema huko?
"Kwema za kutususa? Aliongea mam bakari
" tuyaache hayo hivi huyu ni muda gani toka ametoka hapa? Niliongea kwa sauti ya chini
"Mmh mwenzangu ngoja nikung'ate sikio hata mimi sielewi hapa ndo ameama au ila kiukweli ana muda mrefu hajalala hap muda wote yupo uko ila uja mara moja moja sana" alinifumbua macho sasa
"Nakuomba nikutafute kesho tuongee na ile ishu ya biashara pia tutaijadili"
**********
Nilitazama mazingira yalivyo nikajua kwa hakika kuna watu wameingia pale ndani, nikajua kumbe ile simu ya jana niliyopigiwa na mamdogo kuwa unafanya nini kumbe alipanga kuja kuniangamiza(machozi yakitoka) sikudhani kuwa mama mdogo anaweza kunifanyia unyama huu ila mungu pekee ndio mlinzi wangu. Nilitaka nimpigie simu ila moyo ukakataa, nikairudisha simu kwenye chaji nikawa siamini kila kilichopo ndani, chakula nikakimwaga maana wanaweza kuweka hata sumu, nilitazama kila kona isije ikawa wameweka hata bomu "yani watu awalali wanatafuta roho yangu" niliwaxa cha kufanya nikakosa.
Nikiwa pale nikawaza juu ya ile ndoto nikapata maswali mengi "ina mana hawa watu wamedhamiria kuniua kabisa kama ni hivi inabidi nimtafute elibariki nimuombe msamaha maana ataniua kweli"
(TURUDI KWA CINDY)
Emmy: hivyo ndivyo ilivyokuwa best nikamtafuta elibariki ilikuwa ni jumapili jioni tukazungumza na kuyamaliza mpka leo unaniona hivi
Cindy: vipi kuhusu kaka rafiki na ukweli juu ya mamdogo na salma waliokusaliti?
Emmy: cindy kiukweli sielewi nipo nao peace tu ila kumbo nsyafatilia chini kwa chini maana hata huyu elibariki nipo nae lakini simuelewi elewi yani mguu nje mguu ndani.
Cindy: sawa best mimi naenda basi nina udobi kule hostel si utakuja jioni?
Emmy: sijui mamie namsikiliza shem wako maana weeknd anapenda tutoke sana nadhani anything can happenning sema tutawasiliana.
BAADA YA NUSU SAA.
Nilikaa nikatazama picha zangu za graduation ya form six moyo wangu ulifurahi sana nilikumbuka mengi ila kikubwa isingekuwa kumuomba msamaha elibariki hata kufa ningekufa kwani aliniandama sana 'lakini je ni kweli amenisamehe au ananilia timing aniangamize? Nitajua ukweli kupitia kwa kaka rafiki na mamdogo" nilijipa moyo uku nikizidi kufungua albam yangu nikaona picha ya sam akiwa amebeba beg lake roho iliniuma sana nikaanza kutoka machozi 'sam ni kaka rafiki kabisa ananificha tu kaka rafiki ni sam" nilipata wazo nimtafute maana ni moezi sita imepita pasipo kuwasiliana nae
Kila nikijaribu zile namba hazipatikani kichwa kilizidi kuniuma maana kuna sifa za sam ndani ya kaka rafiki. Wakati napiga namba moja iliyoanziwa na +254 ile simu ilipokelewa lakini hakuwa kaka rafiki, niliongea nae nikajua hakika si yeye.
" dada niko kwa job huyo chalii simfahamu wa kuitwa hivyo' aliongea rafudhi ya kikenya
"Amekuwa akinipigia kwa muda mrefu sana kaka nisaidie"
"Ni muda gani sasa?
" miezi sita imepita"
"Anhaa huyo aitwi kaka rafiki anaitwa abdulrahim alikuwa hapa ila alirudi tz uko miezi kumi iliyopita ila nilisikia tena yupo uku mombasa ila sijapata kumet nae"
Alitaja jina la abdulrahim akanichanganya kabisa
"Samahan kaka yupoje huyo abdulrahim?
" ni mrefu yuko na musculurs/misuli ni mtu wa it na anafanya kazi na shirika moja linaitwa MFS(MUSLIM FREE SOCIETY)"
"Ndio huyo huyo kaka nitakuja mombasa kaka"
"Noo nitakupa web yao uwasiliane nao ila wana matawi duniani hata zanzibar wapo pia" aliongeza yule jamaa
"Sawa kaka naomba nitumie kwa email yangu emmyqueen@gmail.com
Nilimalizana nae nikaketi mezani nikaanza kuwaza ni maswahibu gani yamemkuta sam hadi kubadilisha jina/dini nikaapa nitafanya kila niwezalo nipate details zake zote, nilianza na kumtafuta baba yake kule kijijini.
Nakumbuka nje na elimu yake sam alikuwa ni mtaalamu sana wa computer mambo ya internet na maintanance kitu kilichokuwa kinampa kipato pia cha kuendesha maisha yake ya chuo.
Ilikuwa ni jumatatu niliweza kupata taarifa ya kutoka kijijini kwao na sam kuhusu uwepo wa baba yake, taarifa nilizopata ni kuwa kwa kipindi kirefu baba yake na sam hayupo pale kijijini na wati hawajui alipoenda ila inasemekani yule mzee alipata ugonjwa wa kansa.
Taarifa zile zilinifanya nizidi kuumia inakuwaje hii ikanibidi nifikirie kufunga safari nikamtafute sam huko mombasa ila kabla sijaenda nilichukua laptop yangu nikatafuta jina la hiyo MFS na kazi zao na uongozi wao.
MFS.
dealing with social matters/wanajihusisha na mambo ya kijamii, kujenga shule, visima, misikiti na kutoa sponsors kwa wanafunzi na scholarshp.
>uongozi, meneja musin a musin, ahmed zakir, eli-babu, abdulrahim rahim, rashishi aziz, mohamed omar.
Haya ndio yalikuwa matokeo ya nilichokitafuta nikaangalia majina mawili nikawa na hofu nayo ils nikaapa kuyafatilia kwa kina.
*******""""""""""
ITAENDELEAAAA


USISAHAU KU LIKE PAGE YETU,BONYEZA LIKE BUTTON

No comments:

Theme images by pollux. Powered by Blogger.