NJIA MBILI ZA ASILI ZA KUONDOA MICHIRIZI KWENYE NGOZI YAKO


NJIA MBILI ZA ASILI ZA KUONDOA MICHIRIZI KWENYE NGOZI YAKO

Stretch Marks (michirizi) hutokea sehemu mbalimbali za mwili, mikononi, miguuni, mapajani, tumboni n.k. Wengi hutokewa kutokana na kuongezeka kwa mwili (kunenepa) au ujauzito, hii hutokana na ngozi kutanuka na kusababisha cellulite.

Tatizo huwakumba wanawake kuliko wanaume kwa sababu ya unene kupita kiasi hupelekea lea (layer) ya ndani yenye mafuta kuwa na msuguano na tishu za ngozi hivyo kupelekea mikunjo na michirizi katika ngozi.

Hizi ndizo tiba zake asili (1) MAFUTA YA MNYONYO
Mafuta ya mnyonyo husaidia sana kwenye ngozi kama mikunjo ya ngozi usoni, chunusi, mabaka meusi kwenye ngozi lakini pia husaidia katika kuondoa michirizi.
💚 Paka mafuta ya mnyonyo mahala palipo na michirizi kwa muda wa dakika ishirini kisha jisafishe kwa maji ya uvuguvugu. (2) VIAZI MVIRINGO
Viazi vina vitamini na madini ambayo husaidia ukuaji wa seli za ngozi.
💚 Kata kata kiazi chako katika vipande vyembamba.
Chukua kipande cha kiazi na ukisugue pale kwenye michirizi yako, hakikisha yale maji ya viazi yameingia kwenye michirizi yako.
Kaa nayo kwa muda wa dakika 20 kisha jifute kwa kitambaa au maji ya uvuguvugu. Fanya zoezi hili hadi michirizi iishe.
Somo litaendelea ili kukuongezea maarifa zaidi ya kutibu tatizo hili



USISAHAU KU LIKE PAGE YETU,BONYEZA LIKE BUTTON

No comments:

Theme images by pollux. Powered by Blogger.