Utafiti: Kutokula Kunarefusha Maisha


Utafiti uliofanywa nchini Marekani, umebaini kuwa kutokula kwa saa 16 hadi 18 au kufunga kula kila baada ya muda fulani ndani ya wiki kunarefusha maisha na kuzuia magonjwa kama shinikizo la damu.

Matokeo ya utafiti huo yalichapishwa na jarida la New England Medicine, na kubainisha kuwa kula ndani ya saa sita hadi nane kwa siku na saa zilizobaki kukaa bila kula kunaongeza nguvu ya kinga ya mwili dhidi ya magonjwa.

kwa mujibu wa mamlaka hiyo ya tafiti za kisayansi, kufunga kula ni moja ya njia zinazopendekezwa kwenye matibabu ya kiribatumbo, kisukari na magonjwa ya moyo.

“Inapendekezwa mtu afunge siku mbili kwa wiki au kula kiasi kidogo cha chakula kila siku” imeeleza sehemu ya utafiti huo.


Utafiti huo uliofanywa kwa kutumia sampuli za binadamu na wanyama, umeeleza kuwa kurefusha maisha kunatokana na kuhuishwa kwa chembe hai za mwili.


USISAHAU KU LIKE PAGE YETU,BONYEZA LIKE BUTTON

No comments:

Theme images by pollux. Powered by Blogger.