Chukua hii

Beautiful sexy woman with red lips, nails and rose flower Stock Photo - 32974121
1. Kulala peke yako ni bora zaidi kuliko ku-share kitanda na mtu ambae ana-share kitanda na mwingine pale usipokuwepo.

2. Usaliti si lazima kissing, meeting, au kukutana kimwili na mchepuko. Kama ukijikuta unaweka password, unafuta texts, na wasiwasi simu inapoita mbele ya mwenzako hapo tayari unasaliti.

3. Kama mwanamume ni crazy juu yako, omba Mungu asipate nafuu, kama anapata nafuu, ujue kwamba wanawake wengine wamemuanzishia dozi.

4. Ni kweli penzi la kwanza linaweza lisife (first love may not die), ila ukipata penzi la kweli unaweza kulizika kabisa penzi la kwanza.

5. Kama bado unaamini "PENZI NI UPOFU" ni hakika kwamba "NDOA ITAFUNGUA MACHO YAKO"

6. Sura nzuri ya mwanamke inavutia 'flirters' na 'playboys' bali Moyo mzuri wa mwanamke ikiwemo na tabia njema unavutia 'gentlemen.

7. Kamwe usiingie kwenye mahusiano kwa sababu ya upweke. Ingia katika mahusiano ukiwa na utayari.

8. Ni vema ukaendelea kukaa nyumbani kwa baba yako, kuliko kwenda kukaa kwenye nyumba ya mwanaume ambae huna uhakika nae.

9. Mwanaume hapimwi kwa kuzalisha watoto wengi, kila mwanaume anaweza kuzalisha. Dili la kweli ni wanaume wangapi wanaweza kuwa Baba bora kwa watoto wao pasina kuwatelekeza na mama yao. Hapo ndipo uanaume unapopimwa.

10. Wake walio wema hawaongei tu, wanatunza nyumba zao, wanapika vyakula vitamu, wanalea watoto katika misingi bora na mwishoe huwapendezesha waume zao waonekane kama wafalme.


USISAHAU KU LIKE PAGE YETU,BONYEZA LIKE BUTTON

No comments:

Theme images by pollux. Powered by Blogger.