Mwanaume, chukua hii uishi nayo
Mwanamke anayekupenda kwa dhati, atajitoa kwako kwa kila hali. Unajua, kuna mambo ambayo si rahisi kufanyiwa na kila mtu, yapo ambayo yanafanywa kwa watu wanaopendana tu. Huyu atajitoa kwako, atafanya mambo muhimu ambayo si rahisi kuyafanya kwa mtu mwingine.
Atakupa vipaumbele kwenye mambo yake yote kwa kukueleza mipango yake (hata ile ya siri) na kukufanya wa kwanza kujua kinachoendelea katika maisha yake.
Lazima ujiulize na uangalie, je, wewe ni moja ya vipaumbele vyake? Je, wewe unakuwa wa kwanza kujua mambo yake kabla ya rafiki zake?
No comments: