Chombezo : Dada Emmy (Muuza Ubuyu) Sehemu Ya SITA (6)


Nilikuwa mkimya mno nikisoma simulizi za mejah the plan boy ambaye mara nyingi uandika ktk page yake ya dimbwi la simulizi, kila mara zote anazotoa mwendelezo nimekuwa nikifatilia maana napenda sana fasihi maana ndicho kitu ninachosoma na uwependa kukosoa baadhi ya waandishi ambao hawafati kanuni za kiuandishi na wasiopenda kubadilika. Wakati namalizia kusoma simulizi ya " utamu wa mchezo" nilisikia simu yangu nyingine inaita ya line ya halotel. Nilikimbia fasta kuipokea sikufanikiwa kuigundua ni namba ya nani maana ilikuja bila jina.
"Emmy upo wapi? Ilisikika sauti nzito
" nipo nyumbani wewe nani?
Niliuliza kwa uoga kidogo
"Mimi ni rafiki yako, napenda uniite rafiki" aliongea yule mtu
"Sikujui wewe rafiki umenifahamu wapi?
" hahaaa emmy muuza ubuyu nakufahamu napenda kukwambia kitu emmy" iliongea ile sauti na kuendelea kunitisha
" kitu gani?
" emmy una mkono wa pesa, nyota yako inang'aa na usidhani wanaume wanakutaka bure kuna kitu wanapata kutoka kwako"
Alizidi kunitisha
"Wewe mbona sikuelewi"
" unaweza usinielewe leo ila kesho utanielewa ila kuwa makini kwani huyo elly amefanikiwa mambo mengi kupitia wewe hivyo nyota yako kali sana emmy"
Nilibaki mdomo wazi na kuanza kujiuliza kuna ukweli gani juu ya anayoongea yule kaka rafiki. Nilipoita sikuweza kupata mwitikio kwani simu ilikuwa imekatwa tayari.
Nilijiuliza maswali mengi sana baada ya simu kukatika yule kaka rafiki ni nani? Ila sikupata majibu niliendelea kuwa mpole nikarudi mezani taratibu nikashika simu yangu kubwa ikabidi nizime data maana hapo awali nilikuwa nasoma simulizi za mejah the plan maker.
"Mungu wangu leo tarehe 20 siku zinazidi kwenda karibia nifanye mtihani wangu wa kumaliza kidato cha sita eeh mungu wewe ndiye unajua maisha yangu natamani siku moja nifike chuo kikuu udsm"
Nilikuwa na determinations/matarajio makubwa hasa mbele yangu ni ili la kufika chuo akili na mawazo yangu yalikuwa uko tu. Nilitazama ratiba yangu nilikuwa natakiwa nisome geography, akilini mwangu nilitaka nisome geography2 maswali ila nilitazama mzigo niliokuwa nao geography 01 nikazuta begi langu nikatoa kitabu kilichoandikwa na zisti kamili cha physical geography nikaanza kusoma theories za structure of the earth nilianza na isostancy theory, kisha plate tectonic theory nikajihisi usingizi mzito nikaegemea kwenye kiti nikapitiwa na usingizi, ilikuwa michale ya saa7 usiku.
***************
05:43
Nilishtuka kutoka usingizi ndipo nilipogundua kumbe nilala palepale nikanyanyuka huku nikihisi mgongo unaniuma sana, ingekuwa siku za kawaida ningeenda kulala lakini mitihani inakaribia sikuweza kulala kabisa niliingia bafuni nikawasha maji ya uvuguvugu nikaoga ili mwili upate nguvu kisha nikarejea tena mezani kwaajiri ya kuendelea na ratiba yangu.
Ile asubuhi nilipitia topics za pratical geography hasa map na statistics nilihisi sehemu hiyo ndiyo nilikuwa na mapungufu mno, sikupenda kupoteza muda wangu kuwaza mengine ilibidi nizime simu kisha nisome intensive/kiundani maana kama nikiacha simu on atakurupuka jimmy atapiga au willy na sasa huyu aliyenipigia jana anayenipa stress kumfikiria ni nani/kaka rafiki nae ameongezeka hivyo nikikaa kuwafatisha sitafika mbali au malengo yangu ya kufika university of dar-es-salaam hayatatimia.
Nilisoma sana na niliona raha bado ya kusoma maana kuna raha ukisoma kitu alafu ukakielewa, ilifika saa moja kasorobo nikatoka mezani kisha nikaosha vyombo vyangu na kuanza kufanya usafi nyumba nzima kabla sitoa mapazia na vitambaa kwa ajiri ya kufua. Haikuwa kazi rahisi niliitaji yamkini kupata dada wa kazi lakin naye atafanya nini pale ndani na uku kazi nilihisi naweza kuzimudu mimi mwenyewe. Wakati nafanya usafi nilikumbuka kitu kilichonifanya nikae na kutafakari "hivi mimi nina maadui wengi sana? Ni nani anayeniandama hivi kila siku yanaibuka mapya nina nini mimi? Uenda anachosema kaka rafiki kweli inawezekana nina nyota kali maana sio rahisi wanaume waning'ang'anie mimi tu haya jimmy, willy na elibariki kuna kitu hapa" nilimaliza kuwaza kisha nikasimama na kuendelea na mengine.
**********************
Nilifika eneo ambalo jimmy aliniomba nifike japo nilitoa udhuru nyingi ila alinisihi hata kwa dakika kumi tu kisha nitaendelea na ratiba yangu nilikuwa suprised/shangazwa baada ya kuona duka zuri la nguo za watoto/baby shop za kila aina ambapo pia waliuza sabuni, maziwa ya lactose, pampers na kila kinachoitajika kwa watoto kwanzia mwezi mmoja mpaka miaka 7, kila aliyeniona alishangaa sikuweza kujua kwa haraka haraka wanashangaa nini ila inaonekana ujio wangu ulikuwa tayari umeshajulikana.
Baada ya kuzunguka duka zima jimmy alianza kunieleza baadhi ya mambi kuhusu kazini kwake.
"Unajua emmy wewe ni mwanamke wa ndoto za wanaume wengi, ufanani na mazingira uliyokulia kusema ukweli toka ile siku ya kwanza nilipokuona tukishughulikia suala lako lile(kesi ya sam) nilitokea kuvutiwa na wewe nikamwambia willy naye pia alionyesha kukubaliana nalo ila kumbe naye moyoni anakupenda sikujua, akaamua kuniwahi ila kwangu sikukata tamaa nimeamua kukuonyesha ni jinsi gani nakupenda nakupa duka hili liwe lako bby"
"Wow! Nashukuru kwa kuwa muwazi hata willy pamoja
na kufanya yote aliyofanya hakuwahi nitamkia kuwa ananipenda nakushangaa wewe kwa ujasiri wako" niliongea kwa ujasiri huku namtazama usoni nilimuona akitabasamu.
"Naomba nikubalie emmy"
"Usijari ila kusema ukweli mimi nina mtu ninayempenda yule sam niliyewahi kuwaambia hivyo nisingetamani anione msaliti na hapo badonatoka na elibariki kimakosa sitamtendea haki sam na elibariki eti kisa hawapo na pia utu wangu nitaonekana kama najiuza tu"
Niliongea huku machozi yananilenga.
"Hapana emmy hii itakuwa ni siri kati yetu hakuna atakayejua"
Alibisisitiza sana huku aking'ang'ania mkono wangu
"Hapana jimmy wakina emmy wapo wengu unawexa mpata mtu mwenye sifa kama zangu cha msingi usiwe na haraka ili kumpata"
Niliongea kabla sijaingia ndani ya gari yangu tayari kuondoka
"Pleaseee emmy nakusihi"
Sikutaka kumpa tena second chance nikaondoka
Akili na moyo vikawa vinashindana moyo unasema "chukua duka na alikuahidi nyumba ya kuishi na mama yako mdogo kubali" na akili inaniambia "no kumbuka wema wa elibariki usimsahau sam mtu unayempenda kwa dhati hayo ni yakupita hata kwa nguvu zako utapata siku moja" niliendasha gari nikiwa na migogoro nafsia ni lipi nifanye lipi niache. Mara nikasikia simu yangu inaita ilikuwa kwenye handbeg, moja kwa moja nilijua ni jimmy sikupokea ikaita mara ya pili nikiwa kwenye jam nikapokea ilikuwa namba ngeni.
"Nani mwenzangu"
"Rafiki yako, naitwa kaka rafiki"
"Eeh jamani wewe unanitakia nini lakini"
Niliongea huku nalia
"Usilie emmy napenda kukumbusha hao wanaume sio wazuri kwako jitenge nao" aliongea kaka rafiki
"Kwanini unafatilia maisha yangu wewe mkaka"
"Kwasababu wewe ni rafiki yangu'
" mimi sio rafiki yako nakuomba futa namba yangu"
Nilikuwa mkali kwake
"Sawa ila willy naye ataandaa mtego kwa ajiri yako kuwa makini, jioni njema"
"Kaka rafiki, kaka rafikiiiiii" niliita bila mafanikio
Niliwaza mtego gani ambao willy anataka aandae kwa ajiri yangu sikupata jibu hapo nilikuwa fire nilisikia simu inaita tena. Niliona jina pale willy "inawezekanaje hii" niliwaza kabla sijapokea sasa cha ajabu nilitazama kushoto nikamuona willy kwenye gari la pembeni yangu nilishtuka mno...
Nilitazama pembeni yangu nikamuona willy akaniangalia na kutabasamu huku simu yake ikiita bado , nilikumbuka maneno ya kaka rafiki nikaanza kuhisi jambo juu yake. Mara taa iliruhusu tupite nikapita nikielekea kariakoo niilitaza site mirror sikuweza kuona gari la willy nikajua tumeachana palepale fire, nilipita msimbazi hapo katikati nikaona carpets nzuri za uturuki nilitafuta parking nzuri ili niingie dukani na pia nilikuwa nahitaji nipite bookshop ninunue reviews za masomo yote kwanzia geography1&2, histry1&2, language1&2 na general studies.
"Habari za leo" nilisalimia
"Salama dada karibu" aliitikia muuzaji ambaye alikuwa ni mdada km mwarabu aliyechanganyika na uswahili
"Naomba hiyo carpet ya pink yenye mistari ya reds na purple"
Alisogea kunitolea carpet mimi nilichukua simu yangu na kujaribu kuangalia maana kuna jumbe zilikuwa zinaingia wakati nipo nadrive sikupata bahati ya kuzisoma. Zilikuwa ni nyingi mno kuna wateja wangu wa ubuyu, willy, jimmy na salma zikuzifungua kutokana na muda kuwa mdogo.
"Dada iangalie" aliniita yule mdada kunifanya niachane na simu nitazame yeye.
"Hiyo ni shilingi ngapi dada? Ilisikika sauti nyingine ya pembeni ila bado ckuitilia maanani
" ni laki nne na arobaini ila bei inapungua" alijibu yule dada
"Dada nimeipenda hii nipunguzie" nilijaribu kumuomba hapunguze bei.
"Hii hapa dada nimeshamlipia" aliongea yule kaka nikashangaa mno niligeuka kumtazama vizuri alikuwa ni willy.
Nilibaki mdomo wazi nikashindwa nisemaje kwa muda ule nilimtazama nikamtazama yule mdada muuzaji aliyekuwa anamwambia mkaka mmoja anibebee lile zuria mpka nitakapomwambia aliweke.
"Dada una usafiri? Aliuliza yule mdada sikumjibu bado nilikuwa nashangaa na willy alionyesha tabasamu pana mno ila mimi nikakumbuka maneno ya kaka rafiki " willy atakuandalia mtego kuwa makini" nilipokumbuka hivyo nilimgeukia yule dada muuzaji.
"Dada nashukuru naomba mpeni aliyelipia, willy asante ila sihitaji kwa sasa" nilimjibu willy na kuondoka kuelekea garini.
"Kuna wanawake wasumbufu namna hii" aliongea willy na kuondoka pia kuja upande wangu lile zuria likabaki mgongoni kwa yule kijana.
"Please naomba usinisumbue willy nilihitaji msahada wenu wakati nina kesi yangu, mmeshindwa kunisaidia mnaleta mapenzi mwambie na mwenzako mimi sina njaa kihivyo kama mna moyo wa kusaidia mkasaidie watoto yatima msinisumbue tena" nilimaliza nikafunta gari na kulock milango yote.
Nilihisi kichwa kinauma nikamuitaji sana kaka rafiki angalau anipigie simu anielekeze cha kufanya maana nilihitaji mfariji kwa wakati huu ila ckuwa nae hivyo kaka rafiki nilihisi ni mtu anayenitakia mema mno.
Ujumbe ukaingia niliwahi fasta kuufungua namba ngeni "emmy usirudi kijichi nenda kwa mama temeke" nilijibu
"Kuna nini kwani? Sikuweza kupata tena jibu zaidi ya nusu saa ilipita nikaamua kupiga simu
" namba ya mteja unayompigia haipatikani kwa sasa tafadhari jaribu tena baada, the number..." Nilikata simu kwa hasira
*************
Wakati nafika nyumbani(kwa mama mdogo) nilishangaa watu wakiingia kwenye gari aina ya noah wamembeba mdada aliyeonekana ni mgonjwa sana alikuwa amevaa dela nakumbuka, sikutilia maanani japo watu niliowaona nawafahamu niliendelea kutembea ghafla moyo ukawa mzito nikamsimamisha dada fulani anaitwa mwajuma "samahani kwani yule dada kapatwa na nini?
" haaaaa mwanaharamu mkubwa weee emmy sijawahi kuona mshenzi duniani kama wewe mpaka mama yako anazidiwa anataka kufa wewe ujui unatanua tu na vigari vya kuongwa, chefuuuuuu" aliishia kunishamba niliumia sana kwa yale maneno nikakimbia haraka kuwahi lile noah ambalo mlango wa abiria ulikuwa unafungwa.
Toba yarabi nafsi nilipohitaji kuingia nilipewa maneno ya kashfa ina maana pale mtaani hakuna aliyenipenda hata mmoja "toka tena ukome we mtoto kama umeshindwa kumlea mama yako tuache sisi tutamtunza ndo nyienyie freemason mnatoa ndugu zenu kafara ilo mfanikiwe kimaisha wee emmy wa kuvaa nguo za gharama namna hiyo mama yako hana hata hela ya kula toka sitaki kukuona" nilisimama nikaanza kulia huku nikimkumbuka mama yangu "emmy mwanangu ishi vizuri na wakubwa zako na hata wadogo waheshimu uwezi kujua atakayekusaidia nani, mheshimu mtu bila kujali anamuonekano upi utafanikiwa mwanangu" ni maneno ya mama kabla ajafa nimekuwa nikiyakumbuka ili ili ninalo bambikiwa leo sio.
"Mwajuma ni kweli emmy kamroga mama yake mdogo" nilisikia mnong'ono nikiwa nimesimama pale
"Wee uoni mtaa huu ni nani asiyejua kuwa emmy alikuwa maskini wa kutupwa nakumbuka alikuwa na nguo mbili tu tena gauni na dela muda wote unamkuta emmy na kanga haya ya leo haya kumiriki hadi nyumba, gari na kuvaa minguo ya gharama unafikiri ni nini kama sio ndumba" aliongea mwajuma bila wasiwasi hakujua ni jinsi gani ananiumiza.
"Iki kiama wengu watachomwa moto emmyhuyu alikuwa anakuja kwangu ananiazimisha nguo leo anaringa kisa kigari hicho simpendi huyu mdada hadi kinyaa" aliongea mwanaidi rafiki yangu wa kitambo
Niliendelea kulia hadi kimasi lilianza kunitoka na kichwa nacho kilianza kuniuma.
Niliondoka pale nikasogea hadi nyumbani mlango ulifungwa na funguo hazikuwepo pale nilipokuwa nimepazoea nikija nazikuta, nilimuona mpangaji jirani yetu mama bakari.
"Emmy kulikoni dada?
" shikamoo dada"
"Marahaba poleni ila hali ya mama yako haikuwa nzuri ulikuwa wapi kipindi chote?
Aliuliza mama bakari
" dada mama bakari mimi sijui lolote lile na kusema ukweli natuhumiwa kwa mambo nisiyoyafanya"
" emmy mdogo wangu mtaa mzima umekuwa gumzo wewe unaonekana umemroga mama yako ili upate mali nilivyosikia hivyo niliumia wanadai hata kumsaidia umsaidii chakula tu tuliwekeana zamu hapa kumuhudumia kweli emmy umeamua kufanya hivyo?
*mungu wangu mamdogo unanichumia dhambi bure, angalia mihamala hii nimekuwa nikituma laki kila wiki kweli simjari mama mdogo" nilifungua message na uzuri sikuzifuta sio kwamba nini nilikosa muda na mara ya mwisho aliniomba laki mbili hii niktumia.
"Kheeee kweli jamani mimi juzi hiyo ya.laki mbili aliniomba nimuandikie ujumbe hali yake ilikuwa mbaya"
"Sijui nifanyaje roho inaniuma kusingiziwa, ona message hii hapa namlazimisha aje kukaa pale kwangu unaona alichonijibu.
" mimi nimeshazoea maisha yangu ya temeke, ukitaka wewe mchukue rafiki yako salma uishi naye" ilisomeka hivyo
"Sasa napata picha emmy kuna kitu kinaendelea kati ya mama yako na baba mwenye nyumba na mama yako, na hii nakwambia siri mwisho niliwahi kumuona yule mkaka bonge akiwa nae(elibariki)'
Nilijikuta natokwa na machozi mama bakari alinitazama nikamuona nae machozi yakimtoka akanikumbatia kwa nguvu na kuniambia kwa sauti ya chini sana "emmy mdogo wangu usilie ndio ukubwa huo dada nakuomba wasamehe bure"
"Dada inauma kumbe kila nikipita hapa mtaani naonekana kituko hivi kweli mamdogo anaweza kunifanyia unyama huu"
"Emmy ebu kaa chini nikwambie jambo"
Niliamua kumsikiliza mama bakari nikachukua kigoda na kuketi huku nikimtazama usoni, nae alikaa kwenye mlango wake na kuanza kuongea huku mimi nikiwa bado namtazama ni nini anataka kuniambia.
"Emmy kama kusingiziwa wewe sio wa kwanza, kupitia shida emmy wewe sio wa kwanza na hata kusalitiwa wewe sio wa kwanza, emmy katika maisha yangu nimejifunza kusamehe mpaka hapa unionapo nimetendewa mengi nimesamehe nawe msamehe mama yako" aliongea mama bakari ila bado sikumuelewa kwangu yalikuwa ni maneno ya kawaida.
"Hivi kweli mama mdogo katembea na elibariki kabisa? Niliuliza kwa jazba
" tulia basi emmy mbona hivyo tunaongea wawili tu mbona hivyo"
"Mama bakari nakuheshimu wewe tu ila kile nitakachomfanyia hatasahau ngoja" niilizidi kutoa kilicho moyoni huku kifuani nilihisi kitu kama kiungulia.
"Hivi emmy wanaume unawajua kuliko mimi? Emmy usinione hapa nimepitia mengi kwenye mapenzi nimetendwa na hawa viumbe wanaitwa wanaume nilijuta kupenda niliwachukia wanaume nilimchukia hadi baba mzazi"
"Kheeeeeee" nilishangaa aliposema alimchukia hadi baba mzazi
"Usishangae emmy ndivyo ilivyokuwa"
"Ilikuwaje dada"
****************
FEEDBACK YA MAMA BAKARI KWA EMMY.
(KUMBUKA KUWA HII BADO NI SIMULIZI YA YALIYOMKUTA EMMY AKIMSIMULIA RAFIKI YAKE HIVYO TUWE MAKINI).
Nikiwa msichana mdogo(darasa 6) baba yangu alifukuzwa kazi aliyokuwa anaifanya katika shirika la reli tazara katika mkoa wa tabora. Kipindi hicho tulikuwa tunakaa kota za railway officers. Maisha yalibadili pindi tu tulipoama pale railway kota.
Kipindi kifupi kile mama alianza kufanya biashara ndogo ndogo za kuuza nguo kwenye gurio na mnadani, mimi fatuma(mama bakari) kila niliporudi shule nilikuwa naenda kumsaidia mama katika kuuza biashara yake, mambo yalizidi kubadilika hasa baba alipoanza kunywa pombe kitendo kilichopelekea fedha zote alizolipwa na shirika la reli kumalizika kwa pombe na wanawake..
Nilipomaliza darasa la saba sikubahatika kufaulu kuendelea na elimu ya sekondari hivyo rasmi nilijiingiza kwenye shughuli ndogo ndogo za kuuza vitafunwa na jioni kumsaidia mama mnadani siku zikazidi kwenda, ikafikia kipindi nikavunja ungo na kujiona sasa nimekuwa maana nilichelewa kuvunja ungo tofauti na rafiki zangu. Mara zote mama alikuwa akinihusia usafi(mwili na mazingira) maana tayari nilikuwa mwanamke na kikubwa zaidi juu ya kujiheshimu na kikubwa alinihusia juu ya kuwaogopa viumbe wanaoitwa wanaume.
Nilikuwa nikiyakumbuka mahusia ya mama kwani pamoja na kutongozwa sana na wanaume bado nilikuwa na msimamo, siwezi sema nilikuwa sipendi la hasha nilipenda ila niliogopa mama akijua yale nitakuwa matatizoni hivyo nilizidi kujitunza mpaka nilipofikia miaka 17 ambapo ndio nilipokutana na changamoto nyingi kutoka kwa mzazi wangu wa kiume/baba. Kuna kipndi tulikuwa na mama tunachelewa kurudi nyumbani kutokana na biashara kule sokoni baba alikuwa anamtukana sana mama mbele yangu matusi ya nguoni nilikuwa naumia mno ila sikuwa na jinsi maana nilikuwa mtoto tu kwao.
"Una akili kweli we mwanamke yani mwanao unampeleka kujiuza? Yani kujiuza wewe haitoshi mpaka unamuuza hadi mwanao shenzi sana wanawake ndio maana mimi nasema wanawake wote wasen*** tu" alikuwa akitoa kauli hizo kila siku japo muda tuliokuwa tunarudi ni saa moja jioni tu.
Kutokana na ile hali mama alianza kupata presha na miguu ilianza kujaa maji kiasi kwamba ukibonyeza unaasha alama, kwa mazingira hayo isingekuwa rahisi kufanya biashara hivyo mimi nilisimamia kila kitu nilijikuta nachoka mno maana asubuhi sana namke nikande ngani nipike chapati, maandazi kisha nichemshe chai kwa ajiri ya kwenda kuuza sokoni. Biashara nikimaliza hiyo saa tano asubuhi narudi kuandaa chakula nyumbani na kurudi tena sokoni kuuza nguo mnadani. Kuna wakati nilikuwa nadhurumiwa na wateja wakorofi mda mwingine wanaondoka na hela zangu ila bado sikuchoka maana bila hizo kazi familia yangu haitaishi.
Siku hiyo nikiwa narudi kutoka mnadani nimechoka hoi kuna kijana anaitwa jose alinisimamisha njiani namfahamu ni jirani yetu kwa mama haule nyumba ya tatu kutoka nyumbani. Alikuwa ananipenda muda mrefu huyo jose kipindi hicho yeye alikuwa mwanafunzi wa kidato cha sita mimi ndo kama hivyo nilikuwa mdada tu wa nyumbani. Nilikuwa nampenda jose ila nilimuomba anitunzie heshima yangu tusifanye mapnzi hadi tutakapo kuja kuoana(nilikuwa bikra) alinishika mkono akanipusu na kunikumbatia hapo ghafla baba akatokea nilimuona jose akikimbia kuelekea porini mimi niligombezwa na kupigwa fimbo kama mtoto njia nzima huku nikipewa vitisho "nakwambia utanikoma malaya mkubwa kama mama yako"
Tulifika nyumbani akamwambia mama maneno ya uongo eti amenikuta nafanya mapenzi porini mimi nilishindwa kujitetea mama nae alizidi kunisema nikakosa amani moyoni na tangu siku hiyo baba alianza mambi ambayo sikuyaelewa mara aje chumbani kwangu au aje bafuni nikioga(bafu la makuti) akijifanya kajisahau nilikuwa nikikaa peke yangu nalia mno.
Nilifanikiwa kupata laki moja ambayo ilimuwezesha mama kupata matibabu na kuhudhuria mazoezi kila asubuhi. Jumapili asubuhi ni siku ambayo mama alianza kwenda hospitali yeye mwenyew mimi nilikuwa nje nafanya usafi wa vyombo na kufagia mazingira nikasikia naitwa ndani.
"Fatuma njooo" ilikuwa ni sauti ya baba
Nilirudi ndani kwenda kumsikiliza akaniruhusu niingie chumbani kwake na hapo ndipo aliponikamata na kunichania nguo na kunibaka nilipiga kelele ila sikupata msaada mithili ya kilio cha samaki. Alitumia zaidi ya masaa manne mpka kufanikiwa kunifanyia kile kitendo maana mna wote tulipigana ila baadae alinikaba na kunixidi nguvu, niling'ang'ania chumbani sikutaka kutoka ila mama akirudi anikute palepale.
"Fatuma twende uku" aliongea kama mtu
"Samahani we mwanaume niache unachohitaji kingine kutoka kwangu ni nini? Wanawake siku zote ni dhaifu umetumia nafasi hiyo kunifanyia hivyo ulivyofanya nakuahidi sikuwahi na sitawahi kuwa na baba kama wewe ustahili kuwa baba na raana hii itakusumbua maisha yako yote mpaka unakufa" niliongea maneno kwa uchungu nikatoka chumbani.
Baada ya muda mama nae akaingia nikiwa chumbani najiangalia kweli sina bikra tena, kweli jose ataniamini mimi? "Fatumaaaaa nileteee maji mwanangu"/sauti ya mama ilinishtua nilivaa nguo yangu ya ndani haraka nikatoka ila nilisikia maumivu mno kiunoni na sehemu za siri.
ITAENDELEA


USISAHAU KU LIKE PAGE YETU,BONYEZA LIKE BUTTON

No comments:

Theme images by pollux. Powered by Blogger.