Chombezo : Dada Emmy (Muuza Ubuyu) Sehemu Ya NNE (4)


Baada ya kumaliza shughuli zangu zote kiukweli nilikuwa nimechoka ila ilinibidi nisome vitu viwili kabla sijalala kwanza nimalizie kukisoma kitabu cha "i will marry when i want" na nifanye maswali tuliyotolewa na mwalimu ya topic ya "rise of democracy in europe" history2.
Nilifanikiwa kujibu yale maswali yote ila nilishindwa kumalizia kusoma ile play ya "i will marry" kutokana na kuanza kusinzia, "mmh ila huu usingizi jamani ndio kwanza ni kitabu changu cha pili kusoma bado novels bado poetry nikizembea nitafail bure inabidi nijikaze mno" wakati najitafakari niliamua nilale hivyo nilienda kuchukua simu niliyoiweka kweny chaji muda mrefu kidogo nikaiwasha..
Haxikupita dakika tano ile namba ikaingia tena "jamani huyu nani mbn sielewi itakuwa ni yule aliyeniingizia milion kumi kweny akaunt yangu au freemason? Nitamwambia haitoe hela yake" nilipokea kwa ujasiri
"Hello nani mwenzangu"
"Emmy mambo"
Nilipigwa na bumbuwazi ghafla sauti ya elibariki kimaro au sweetmangi sikuamini.
"Vipi mbona kimya?
" hapana nakusikiliza"
"Naomba sahau yaliyopita bby, niambie masomo yanasemaje?
" namshukuru mungu"
"Nimekuingizia hela kweny akaunti yako na kuna gari nimekuagizia kutoka japan nimeshaikatia kila kitu kwa hapi nchini mimi nipo south africa uko nitarudi mwisho wa mwezi huu nakuomba kuwa makini*
" wow! Nashukuru baby asante" nilitepeta mwenyewe niliposikia gari na milion kumi juu umaskini ndo nauasha taratibu na tena hizi shughuli zangu nahitaji mno gari.
"Ngoja nakutumia picha za hiyo gari whatsapp halafu nakuomba urudi kijichi ile ni nyumba yako na nilikutoa temeke makusudi sipendi upate shida emmy"
"Asante honey"
"Jitahidi usome hiyo milioni kumi nimekutumia ufungue biashara sio unaishiwa hata hela ya kuweka mafuta kweny gari au kufanya service"
Niliona ni muujiza mkubwa kwangu elly huyu hata sijui ana akili gani ila ananipenda sana tatizo kwangu ni sam nae ana mipango ya ndoa na mimi soon atakapomaliza masters yake ya mambo ya ukemiia atakuwa na kazi nzuri na yenye kipato kizuri tu.
*****************
Nilikosa majibu ya kufanya maana hawa wanaume wawili wananiumiza kichwa sam nae alikuwa anamaliza field wikii hii tulipanga twende kwao kumsalimia baba yake tumpelekee na zawadi angalau aanze kula matunda ya kuzaa. Ila sasa mimi sam atanitambulishaje kwa baba yake?
Wakati huohuo mwalimu wa language one aliingia darasani akawa anaendelea kufundisha topic ya writing skills nilikuwa nampenda maana nilikuwa namuelewa mno na test zake nilikuwa nafaulu kuliko mwanafunz yeyote mule darasani. Kamwe sikuwahi kufikri kama nitakuja kuikosa amani kwa sasa ila jambola mapenzi ndio ulikuwa mtihani mkubwa kwangu.
*******************
Nilitoka dar na basi la asubuhi ili niwahi kufika morogoro mapema ambapo ndipo tulipanga tukutane sam hivyo nilipofika morogoro terminal sam alikuja kunipokea kisha tukapanda jingine costa kuelekea kweny mashambaya sukari tuliani huko.
Kupenda ni kitu cha ajabu sana elly pamoja na kunisaidia kote kule sikuwahi kwenda kwao hata siku moja na huku wazaz wake wapo dsm ila nimeenda morogoro kwao na sam, baba mkwe alikuwa mzee lakin wa makamo alikuwa bado ana nguvu zake uwezi amini alilima shamba kubwa mno na kupanda miwa, maboga, karanga.
"Karibu sana mama"
"Nashukuru sana"
Tuliongea sana na ninashoshukuru tulienda jumamosi isingeweza kuathiri shule na biashara pia alitoa nasaha zake na kukua ana kiona mbali/hekima alituhasa tujue ni njia gani njema ya mafanikio ya kupita ili tusije kupoteza malengo na ndoto zetu akatupa simulizi za zamani alipokutana na mke wake/mama sam.
"Yeye alikuwa darasa la pili(mama sam) mimi nilikuwa darasa la nne tena nikiwa kaka mkuu pale nilikuwa safi suruali safi, raizoni yangi inang'aaa mabinti wengi walinipnda ila mama yenu nilikuwa namtania siku moja nitakuoa monica kalikuwa kanacheka tu ila nilipomaliza shule nilienda nairobi kusoma huku nyuma nikasikia anataka kuolewa na jamaa mmoja mfanyakazi serikalini na anapesa zake niliamua kuandika barua nikamkumbushia ile ahadi ndo unaona hawa wakina sam leo maana nilimpenda monica na sikutaka kumpoteza japo sikuwa na pesa kama yule jamaa ila nilikuwa na msimamo na nilijua kusimamia ahadi zangu wewe jiukize kenya airway kuna warembo wangapu niwaache nimfatilie binti wa kijijijni?
Wote tulicheka ila ule ujumbe kwetu ulihusika mno nilimkanyaga sam akaniangalia na kunikonyeza, tuliongea mengi mpka muda wa kulala ulipofika tukaenda kulala.
********"""""""""""""""**********
Siku zilikatika elly akarudi tukawa bega kwa bega akitoka hapa nipo nikitoka hapa nipo ila kuna kipnd nilikuwa naangalia nikipata nafasi nachomoka namtafuta sam tunaenjoy kisha ratiba nyingine zinafata.
Nakumbuka siku hiyo nilimpigia salma simu na kumueleza ratiba zangu "shoga fanya fatilia madeni na kama watahitaji mzigo utanijulisha mimi nipo na sam tunaelekea royal hotel kuna mambo ya kibiashara pale".
*****************
" sam nitalipia hapa kwa siku mbili utakuwa hapa siku ya tatu ndo utaondoka sawa baba
"Poa haina noma"
"Baby relax nataka tuenjoy mapenzi sawa?
" aisee hii hotel kweli five stars yani km nipo ulaya"
"Haaaaaaaa its normal ni sehemu ya hadhi yko baby"
*********************
Sijui ni nini kilitokea usiku ila nilijikuta nipo chooni nikiwa uchi nimefunikwa shuka tu nililia mno baada ya kuona michirizi ya damu kweny sakafu na sam sikumuona.
Nilijivuta kutoka kwenye choo na niligundua kuwa mwili haukuwa na nguvu japo sikuwa nasikia maumivu yeyote mwilini mwangu zaidi ya mwili kutokuwa na nguvu tu.
Nilifanikiwa kufikia simu nikapiga costumer care angalau nipate msahada wa kufahamu tukio lile limetokeaje tokeaje na tulikuwa wawili mwenzangu yupo wapi.
"Yes ndugu mteja tukusaidie nini?
Ilisikika sauti ya kike.
" naitwa emmy mejah nipo chumba no:104 nimepata tatizo la kuvamiwa na nilikuwa na mpenzi wangu simuoni na chini kuna michirizi ya damu halii hii inaniogopesha dada yangu naomba msahada"
"Sawa dada tutatuma watu muda si mrefu kwa ajiri ya uangalizi, je kuna uharibifu mwingne umetokea?
Alivyoongea hivyo akanikumbusha niangalie pochi yangu na niligundua kiasi cha pesa nilichokuwa nacho kilikuwepo nikatafuta nguo alizovaa sam sikuziona kikubwa niliona kitambulisho chake cha chuo inaonekana kilikuwa njee na nguo zake ambapo pembeni pia kilikuwa na driving licence " no dada mimi nina kila kitu tatizo ni huyo mpenzi wangu sijui nini kimemkuta aah dadaaaaa" nilianguka na kupoteza fahamu.
**************
TURUDI KWA EMMY NA CINDY.
"Daaa jamani emmy pole sana baby wangu"
"Ndo hivyo ila bado sikata tamaa namtafuta bado sam wangu alikuwa ni mtu muhimu sana kwangu"
"Mmh nimesahau sasa baada ya kuanguka kule hotelini ilikuwaje??
TUENDELEE NA EMMY FEED BACK.
Nilijikuta nipo hospital nikiwa nimetundikiwa dripu huku pembeni walikuwa maofisa wa ile hotelin nahisi wao ndiowalinileta pale. Baada ya dokta kuja aliwapa maelezo machache juu ya hali yangu nami wasaha huo ndio nilipata kujua ni nini kilinikuta (wale maofisa waliact kama ni ndugu zangu).
"Mgonjwa wetu anaendelea vizuri nafikiri leo mchana mnaweza kuondoka nae, ila kilichokuwa kinamsumbua inaonekana alivuta hewa mbaya mfano wa madawa ya kumaliza ya kupoteza fahamu sasa madhara ya dawa hizo kwanza uathiri mfumo mzima wa upumuaji na pia umfanya mtu huyu kuwa unconsious(asij
itambue), kupoteza nguvu za mwili na madawa haya ukaa ufanya kaxi takribani dakika 10-15 au zaidi"
"Sasa kwa hali ya mgonjwa wetu alikuwa affected kwa kiasi gani?
" aaah mgonjwa wetu huyu yeye pamoja na ili alikuwa na upungufu wa maji na inaonekana anapata muda mdogo wa kupumzika kwahiyo ningependa kuwashauri mxingatie sana haya ninayowaambia inabidi apate muda wa kutosha wa kupumzika na anywe maji mengi na si lazima yawe maji tu mnaweza kumpa juice na matunda kwa wingi".
Nilitafakari sana yale aliyokuwa anazungumza dokta na kweli nilikuwa sina mudawa kupumzika yani kwa masaa 24 ni masaa 4 ndio napumzika 20 yote kichwa kipo busy na shule, biashara, mapenzi na familia.
Tulifanikiwa kutoka hospitali saa tisa alasiri wale watu walijitambulisha kwangu kama Jimmy John meneja msaidizi wa mambo ya masoko na William Charles yeye alikuwa ni mkuu wa usalama pale hotelini.
"Sasa dada emmy tunahitaji kufanya mazungumzo nawe sijui ungependelea sehemu gani ya kufanya mazungumzo nawe?
" mmh kwakweli kwa leo sipo sawa naomba niwatafute baada ya siku ya leo"
Tulifanya makubaliano na kisha kuchange contact na walinisihi lile jambo nisiliriripoti police hadi hapo nitakapo kaa nao ila kwa ninavyojua mimi kuwa likitokea suala kama lile la utekwaji nyara, mauaji au ugomvi inapaswa jambo hilo litolewe taarifa ndani ya saa 48 hivyo sikuwa na wasiwasi sana kwani mpk kesho ndio masaa hayo 48yatakuwa yametimia. Walinipeleka mpka nyumbani kijichi ila sikuwa na amani maana nilipofungua tu geti nilihisi uoga wa hali ya juu.
"Mmh au niende temeke? Lakini mara ya mwisho niliondoka na sam nikiulizwa sam yupo wapi nitajibu nini? Aah nitakaa hukuhuku ila nitalalaje peke yangu? Nilijiuliza na kujijibu mwenyewe na muda nao ulizidi kwenda.. Kichwani likaja jina la salma ila nilipolikumbuka nilikosa amani ghafla.
**************
Nilishtuka baada ya kijua kikali kuniunguza miguuni mwangu ambacho kilipitia dirishani nakumbuka hiyo jana usiku nilisinzia palepale sebureni, kitu cha kwanza nilikumbuka simu yangu ambayo niliizima toka nikiwa hospitali sikutaka elly anitafute maana sikutaka ajue nimi imetokea japo nilikuwa na maswali mengi juu ya uhusika wake ktk hili swala la sam. " sijui niwashe simu? Hapana elly atanipigia siwezi kuwasha simu jambo mambo yangu yatakwama kule salma biashara na wale watu wa hotelini niliopanga kuonana nao leo"
Nilijiandaa nikaoga nikawa nafikiria niondoke na gari yangu au nifanyaje?
*********
Nilifika pale hotelini kwakuwa sikuwa na simu ilibidi niulizie kati ya yale majina ya jana pale reception. Nilielezwa ofisi ya jimmy james baada ya yeye kupigiwa simu na kuconfirm niende nikaonane nae.
"Eeh dada emmy karibu sana"
Niliingia ofisini kwake kulikuwa amazing sana computers za hatari malumalu nzuri na air condition safi juu picha ya mkuu wa hiyp hotel na picha ya rais wa tanzania mheshimiwa jakaya kikwete ilikuwa imepamba ofisi nzuri ya jimmy james ambaye inaonekana anakaimu kiti katk ile ofisi.
"Nashukuru kaka, vipi yule kaka mwingine" nilimkumbushia juu ya william ambaye pia tulikuwa wote hospitali jana, alinyanyua simu na kumpigia mimi muda huo nilikuwa naangalia wingi wa vile computer mule ndani.
Muda punde william nae aliingia
"Eeh dada emmy karibu sana, sasa inabidi mheshimiwa ili jambo tukaliongelee ofisini kwangu kule"
Tulitoka wote watatu tuenda ofisini kwa william muda ambapo tulipanda lift kuelekea juu zaidi. Tulitumia sekunde 30 tukatokea ilipo ofisi ya william sote watatu tukaingia ndani tayari kwa majadiliano.
**************
"Emmy umeona huyu mtu unamtambua?
Aliongea sam akimvuta mwanaume ambaye alichukuliwa na cctv ya pale hotelini japo sura haikuonekana ila alikuwa ni mwanaume mweusi mwenye mwili mkubwa william aliama na kwenda camera ya pili na ya tatu hadi ya nne atuweza kumtambua yule mtu zaidi ya sura yake kujificha na inaonekana alikuwa anajua kuwa pale palikuwa na camra za usalama alijitaidi kukwepesha sura mpk mwisho hatuweza kumuona yeye wala sam aliyepita kweny uso wa camera.
" hii ni kubwa emmy sasa tunafanyaje willy? Aliongea jimmy
"Nimekaa zaidi ya masaa manane kufatilia hili ila sijapata jibu sasa tuliacha ili itakuwa ni hasara kwako emmy na kubwa zaidi kwangu ambye ndo mkuu wa usalama hapa" aliongea william akionyesha kuchanganyikiwa
"Sasa emmy nikuulize kitu kimoja wakati unakuja hapa ni watu wangapi walikuwa wanalijua hili?
Aliuliza jimmy.
" nina rafiki yangu anaitwa salma pekee anajua"
"Anhaaa una ugomvi nae labda au mliwahi kukwaruzana hapo awali?
Alidakia william
" noo sijawahi kugombana nae"
"Sawa unajihusisha na nini hapa mjini na huyu rafiki yako anafanya shughuli gani?
Aliendelea william kuniuliza
" mimi ni mfanyabiashara za ujasiriamali na salma ni mtu ninayesaidiana nae"
"Sawa sasa salma ana ukaribu gani na mpnzi wako(sam)"
"Yani tunaishi wote mtaa mmoja ila sam tumepanga sehemu moja ila kwa muda nimekuwa sipo hapo nimeamia kijichi kule uwa naenda pia(temeke)
" ahaa sasa unahisi au uliwahi kuhisi km salma anampenda sam?
"Sikuwahi kuhisi kwani awaha ukaribu kabisa"
"Uko kijichi unaishi na nani na temeke ulikuwa unakaa na nani?
" mmmh kijichi nilinunuliwa nyumba na mpenzi wangu mwingine anaitwa elibariki kimaro na temeke ninaishi na mama mdogo wangu ambapo sam ni jirani yetu"
"Hapo naanza kukuelewa je sam na huyu elly vipato vyao vipoje na wewe una ukaribu zaidi na yupi kati ya hao wawili?
" sam ni mwanafunzi wa chuo kikuu mlimani na elibariki yeye ni mfanyabiashara, ila amenisaidia sana kiuchumi ila hapo kabla nilikuwa nimeshanza mahusiano na sam hivyo nipo nao wote ila nampenda sana sam"
"Salma ana ukaribu gani na elly?
Nilichukua muda kulijibu lile swali kwani nilianza kufikiria jambo ambalo liliwahi kutokea huko nyuma.
TURUDI NYUMA.
(Simulizi ya emmy kwa william na jimmy)
Nakumbuka kuna siku nilikuwa nimetoka shule sikuwa nimewasiliana na salma muda mrefu kutokana na ratiba zangu za shule na pia kuamia kwangu kijichi kulinifanya nikose time kabisa. Siku hiyo nilimua kupitia temeke nikaona sio mbaya nipitie kwao na salma nilikuwa dirishani kwa salma nikijaribu kumtisha ile nachungulia nilimuona salma kalala kitandani anaongea na simu nilifanikiwa kusikia maneno machache " na ukitaka kujua mengi kuhusu yeye nitakwambia ila naomba na mimi unitafutie kazi yani analinga sana siku hizi mmh wenye mapenzi yao"
Nilijua anaongea na shoga yake maana salma kwa kuuza ubuyu hajambo nilimuita ila alishtuka saba akakta hiyo simu aliyokuwa anaongea nayo.
Tuliongea mengi nilikumbuka kuna vocha nilirushiwa na rafiki yangu nikiwa shule kama tarakimu tu ilibiidi nitafute mahali pa kuzinakiri ili niingize.
"Salma niazime simu yako mara moja"
Nilipoishika tu ile simu ujumbe uliingia nikaufungua kwa bahati mbaya "mbona umekata simu sasa ila akikisha unafatilia nakutegemea na unajua mimi huyo mwenzio nampenda sana" nilishtuka nikiitazama ni namba ngeni amby aikusaviwa ilikuwa ni voda ya elibariki kabisa hapo nilishangaa ila aliposikia mlio wa ujumbe kuingia alinipokonya simu yake...
Niliishia kushangaa kwa lile jambo ila sikutaka kulifatilia tuliendelea na story nyingine kisha niliaga na kuondoka japo yeye alikuwa anajishtukia mno.
"Emmy nikusaidie mkoba basi"
Nilimshangaa maana si kwa kujibaraguza kule ila sikuwa na time nae nilimkatalia tu. Na kumbuka hapo nilikuwa nafikiria nimpate mtu wa kuishi nae kijichi anisaidie hata usafi maana nyumba ni kubwa mno na nipo alone(mpweke) nilipoona zile dalili za salma niliogopa kumsogeza karibu na nyumbani kabisa.
*****************
TURUDI KWENYE UHALISIA (OFISINI KWA WILLIAM NA JIMMY)..
"Kumbe ndivyo ilivyokuwa? Willy unaona this is the game for real willy(willy huu ni mchezo kabisa)"
Alihamaki Jimmy
"Yeah ila kuna vitu vya kunote pia, sasa unasema mtu wa mwisho kuwasiliana nae alikuwa ni salma? Aliuliza william
" ndio"
"Na mpenzi wako huyo mwingine(,eliba
riki) uliachana nae muda gani?
Aliendelea kuuliza willy
" kwakuwa ilikuwa ni jioni na mimi na elibariki muda mwingi tulikuwa close aliniambia ndani ya siku mbili hizi atakuwa busy kuna mambo anafatilia ila baada ya hizo siku atanitafuta hapo ndipo nikapata upenyo wa kumtafuta sam tukaja hapa sasa nikiwa najiandaa nakuja nilimjulisha salma haya yote"
"Asante sana kwa kutuambia ukweli sasa emmy tunakuahidi kulifatilia hili jambo ila tunakuomba kuwa mvumilivu sana na usimwambie mtu juu ya hili maana wewe utakuwa hatiani na sisi pia"
Alinitahadhari william.
"Sawa nimekuelewa kwahiyo polisi nisiende?
" emmy hili suala tuachie sisi, sisi ndo tutajua tuanzie wapi na tuishie wapi cha msingi mawasiliano"
Aliongea willy.
"Napenda kukukaribisha tena kupata huduma zetu pia tunakupa ofa ya kutembelea hapa bure kwa six months pia tutakupa kiasi kidogo cha fedha kwa usumbufu uliojitokeza na pole ya kumpoteza mpnzi wako"
Aliongea jimmy kwa bashasha.
"Sawa nashukuru"
"Ukitoka hapo nje kwa cashier(mhasibu) utachukua mzigo wako au kama una account tunaweza kukuingizia bank kabisa"
"Wote kwangu ni sawa tu"
************************
TURUDI KWA CINDY NA EMMY.
"Daah emmy pole mwaya story yako inasikitisha sana"
Aliongea cindy.
"Ndo hivyo imeshatokea nitafanyaje?
" sasa vipi hao wakina jimmy walifatilia hilo jambo la kumpata sam? Na nini elibariki alitambua jambo lolote?
Aliendelea kuhoji cindy.
"Dah shoga we acha tu mambo yalizidi kunisumbua kichwa"
***************
(ENDELEA NA EMMY FEED BACK KWA CINDY)..
Nilitoka pale hotelini nikapokea kiasi cha shilingi milioni nne kwa ajiri ya usumbufu na pole huku nikihadiwa jambo lile kufatiliwa kwa kina.
Niltoka pale hotelin nikapitia bank nikakuta imefungwa hivyo nikabidi niingize gari sheli nikajaza mafuta ya elfu20 kisha nikaanza safari ya kuridi nyumbani, nilipofika mtoni kwa aziz ally nikaingia kushoto kwenye supermarket ya al jazeela nichukue baadhi ya vitu na niulizie fedha za mzigo uliwahi kuletwa pale.
"Karibu dada emmy"
Mhudumu alinikaribisha maana nilikuwa nimezoeleka sana pale.
"Asante mambo naona mpo"
"Tupo karibu mwaya"
Alijibu yule mhudumu anaitwa zenabu.
"Hivi Zenabu nawadai nyinyi"
"Yeah ila bosi alikuja hapa jana akaasha maagizo"
Aliendelea zenabu.
"Mmh maagizo yapi?.
" anasema uache account number ya bank ili tuwe tunafanya malipo kwa bank au tigo pesa ama airtel money"
Nilimuandikia akaunti namba yangu kisha nikachukua vitu pale maziwa ya kopo(nido), penertbarter, mikate, siagi, sukari 5kg, tambi pakti4, mchele kg10, cocoa na juice za pineaple kisha nikafanya malipo nikawa natoka wakati natoka kuna mkaka ambaye ni customer care(mhudumu) alinisaidia ile mizigo kuingiza kwenyr gari. Nikiwa sina ili wala lile nilisikia naitwa "emmy weee emmy" haikuwa sauti ngeni masikioni mwangu niligeuza shingi kutazama daaah alikuwa saleh mpnz wangu wa zamani tulisoma nae shule ya msingi.
"Vipi emmy mambo? Alinisalimia saleh pemben akiwa na marafiki zake.
" poa wapi hiyo?
"Nimetoka chuo hapo TIA(UHASIBU)"
aliongea kwa kujidai kweli.
"Wow! Hongera kweli noe umeamua kusoma maana nilisikia story zako mara ulipelekwa shule uganda ukatoroka, kenya napo ukafukuzwa ila nafurahi kusikia unaendelea na shule"
"Aah waongo tu hao mashilawadu tu me sijafanya yote hayo"
Kabla sijamjibu yule kaka customer care aliniita "dada emmy tayari"
"Nashukuru kaka"
"Karibu tena"
Alipoongea vile nilibonyeza lock kwenye gari kitendo kilichomshangaza saleh na rafiki zake.
"Emmy its your?(emmy ni lako?)
" its mine saleh why not?(ni langu saleh kwanini isiwe?
Tulizungumza mengi akaniomba namba yangu nikampa na kwakuwa nilikuwa na haraka niliagana nae nikampa hela ya soda (30000) kisha nikawa nageuza gari nikamsikia akiwaambia rafiki zake.
"Ebhanaa kweli haya maisha hayana formula huyu demu nimeshamto**** sana na kwao nakujua temeke mikoroshini anaishi na mama yake mdogo dah eti leo ana mkoko(gari)"
"Hahaaaa saleh mwanamke sio mwenzio yeye ana mtaji wewe una nini, cha msingi pasua hiyo hela kati kwa kati tukapige viroba" aliongea rafiki yake wa pili.
"Weee boya kweli unataka hela usiyoifanyia kazi mimi ni huruma zangu nikupe au nisikupe" alijihami saleh.
"Haaa wewe umeifanyia kazi gani?
Aliuliza rafiki yake wa pili aliyekuwa kimya.
" mimi nilimtomb*** vizuri hivyo nimeasha mhuri wangu na kwa taarifa yako mimi ndo nimetoa bikra kwa huyo demu unayemuona"
Sikutaka kusikiliza zaidi nikaingiza gari barabarani hapo kichwani nilinote vitu viwili vikubwa kutoka kwa wanaume "kwanza wengi wao wanapenda miteremko wamkute demu ana mali zake ili wafanye matanuzi ti, pili wanatuchukulia wanawake sisi ni dhaifu sana kwao hasa kwa wale wanaotutoa bikra" niliona ni mawazo ya kijinga ya wale vijana na wengi wao wanakula kwao hivyo hawakuwa na mawazo ya kutafuta maisha zaidi ya kupiga viroba(pombe za mifuko ie zed).
Nilipofika nyumbani niliwasha simu yangu(baada ya siku mbili kuwa off) ziliingia message nyingi mno na mimi ni mvivu kujibu message kwa sababu message nyingi ni za wanaume kukutongoza tu tena wengine ni watu na heshima zao na wengine ni hawa ninaofanya nao biashara, walimu, wanafunzi wenzangu basi ni uchafu. Unajua msichana ukiwa na kipato angalau kama mimi hivi emmy wanaume wengi watakuja ili mradi wapate unafuu wa maisha na wale mabosi zangu ambao nafanya nao biashara wao ni tamaa za kingono wakiona mwanamke mzuri wanamtamani na ndio maana rushwa ya ngono maofisini ni ngumu kuisha kutokana na aina ya mabosi tulionao.
Nikiwa napika jikoni simu yangu iliita nikajifuta mikono na kitaulo ili nipokee alikuwa ni salma.
"Yes salma"
"Mambo vipi emmy?
Ilisikika sauti ya salma
" poa niaje?
"Poa upatikani wangu siku ya pili hii uns nini tena'
" nilikuwa na shida flan ndogo tu lakini, vipi ulifatilia pesa za madeni?
"Aah pole mwaya, ndio nilifatilia kote na jana tulitengeneza mxigo mpya" alijibu salma.
Ahaaaa sawa kesho tutaonana basi"
"Sawa ila nina shida ya laki naomba nisaidie"
"Kheeee jamani salma unapeleka wapi hela juzi nimekupa elfu themanini salna shoga yangu hatuendi hivyo"
"Sio hivyo nina shida hapa sina hata mia"
"Sawa nakutumia"
Nilikata simu nikawaza juu ya salma "unajua salma anataka kuiga maisha yani sijui kwanini ajifunzi kutoka kwangu mimi bank nina karibu milioni 20 ila uwezi kunikuta nafanya matumizi ya ovyo ika yeye atataka ajionyeshe ana hela ikitoka nguo hii yumo hii yumo na hapo hajui km najua anahonga wanaume dah! Alafu kanidanganya kaenda al jazella kumbe ni uongo hajaenda subiri tutachukiana tu maana si kubebana huku na amesahau juzi kasababisha hasara ya laki mbili kunidanganya kaporwa hajui yote nayajua, mimi emmy najua maisha ya kila namna na sitabiriki ni samaki wa maji chumvi au maji baridi sasa we muache anikariri kama samaki wa maji baridi atashangaa ya karne"
Niliongea kama mwendawazimu. Mara sweetymangi(elibariki) nae akapiga nilifikiria kuipokea simu ila nilipokea tu.
"Mambo bae"
"Poa sweetymangi wangu"
"Emmy ulikuwa wapi jana na leo?
Aliuliza kwa ukali.
ITAENDELEA


USISAHAU KU LIKE PAGE YETU,BONYEZA LIKE BUTTON

No comments:

Theme images by pollux. Powered by Blogger.