Chukua hiii...........................

Image may contain: 2 people, people sitting
Mtu anavyokufanya ujione kama HAKUHITAJI basi usiondoke kwake ili ajihisi hatia au asikitike maana hilo haliwezi kutokea.
.
Ondoka katika maisha yake kwa sababu kubwa moja tu, kwamba hujaona sababu yoyote yakuendelea kuwa na yeye au inayokufanya upiganie mahusiano hayo.
.
Inafika kipindi mtu lazima uwe na ujasiri dhidi ya hatima ya maisha yako kwa sababu jambo ambalo umeandikiwa kuwa nalo litakuwepo na kama hukuandikiwa haliwezi kudumu.
.
Ndio, Mahusiano yanafaa kupiganiwa lakini sio wewe peke yako unaetakiwa kupigania. Muda mwingine mtu unayempigania na yeye lazima azione jitihada zako na kuzithamini walau hata kidogo.
.
Kama hana muda huo, itoshe kutambua kwamba unachompa ni zaidi ya anachostahili.
.
Kuwa sehemu ambayo moyo wako unahisi unathamimiwa, jitihada zako zinaenziwa na mchango wako unatambulika. Sio sehemu ambapo unavumilia.

“Don’t try to force anything. Let life be a deep let-go. God opens millions of flowers every day without forcing their buds.”


USISAHAU KU LIKE PAGE YETU,BONYEZA LIKE BUTTON

No comments:

Theme images by pollux. Powered by Blogger.