JE HAYA NI MAPENZI!! 112:





Hivyobasi akaamua kulisukuma na kuingia ndani.
Akashangaa kumuona mlinzi wa Sam akiwa chini huku damu zikimtoka.
Jeff akashtuka sana na kutamani kumsogelea ili amtingishe na kuona imekuwaje.
Ila kabla hajafanya hivyo, moyo wake uliingiwa na mashaka na kumfanya asite kwenda kumgusa yule mlinzi.
Akaamua kutoka nje ili ajaribu kumpigia simu Sam na kumuuliza.
Ila alipotoka nje, akashangaa kumuona yule mlinzi wa Sam akiwa amekaa pembeni ya geti kwenye kiti kama kawaida yake.
Hapo ndipo palipomfanya Jeff apatwe na mashaka zaidi na kujikuta akianza kukimbia.
Yule mlinzi nae akamshangaa na kuanza kumkimbilia ila kitendo hicho ndio kilichozidi kumpa Jeff hofu na kujikuta akiongeza mbio kushinda mwanzoni.
Yule mlinzi aliamua kurudi tu kwani hata hakuelewa kuwa ni kitu gani kimemfanya Jeff akimbie kiasi kile kwakweli hakumuelewa kabisa na akarudi kwenye kiti chake kukaa.

Yule mlinzi akatafakari kidogo kuwa Jeff sio chizi hata akimbie kiasi kile na kuhisi wazi kuwa lazima kuna kitu tu ingawa hata yeye hakuingia tena kwenye nyumba ya Sam tangu siku ile walipotoa mwili wa yule mzee.
Akatamani akachungulie kuwa kuna nini ila akasita kidogo kisha akajiuliza,
"Hata hivyo, amepitaje pitaje huyu bila ya mimi kumuona jamani? Au muda ule nilipozunguka nyuma kidogo?"
Hakupata jibu ila akaona wazi kuwa kwa tukio hilo ni ushirikina ambao umechukua nafasi mahali hapo.
Naye akasita kuingia ndani na kuamua kubaki hapo hapo nje.

Jeff alikimbia hadi kituo cha daladala kisha akapanda daladala na kurudi kwao.
Njia nzima alikuwa akitafakari kile ambacho amekiona, alikuwa akijiuliza maswali bila ya majibu kuwa kitu kama kile kinawezekanaje,
"Ile nyumba ni mauzauza siku hizi halafu Sabrina naye kaenda huko huko, hivi kwanini hajihurumii jamani!"
Akapata wazo la kumtafuta Sam hewani ili aweze kumuuliza kuhusu jambo lile ila simu ya Sam iliita tu bila ya kupokelewa na kumfanya azidi kupatwa na mashaka dhidi ya wakina Sabrina na kutamani hata Sabrina angekuwa na simu basi angempigia moja kwa moja.
Ikabidi arudi tu nyumbani kwao na moja kwa moja akaenda chumbani kwake ili apate utulivu na kutafakari.

Kwa upande wa Sam na Sabrina ilikuwa furaha tu kwani Sabrina alifurahia sana ile nyumba mpya aliyopelekwa siku hiyo na kujiona kuwa ameridhika sana.
Sam alimuaga kidogo Sabrina kwa muda huu na kwenda zake mjini.
Sabrina alibaki na watoto wake, akawaangalia walivyofanana na Jeff akafikiria na stori ya Sam.
"Ingawa Sam hakunimalizia story yake, ila inaonyesha wazi kuwa bila ya Jeff hata mi ningekuwa katika mlolongo wa wadada waliokufa sababu ya Sam."
Akatafakari pia kauli ya Sakina kuwa yule Aisha ni mchumba wa Jeff,
"Mmh huyu nae anataka kuniumiza moyo tu, najua anatamani sana kuujua ukweli ila tatizo ni kuwa akigundua huo ukweli nitaweka wapi sura yangu jamani?"
Aliamua kutulia tu kwani aliona wazi kuwa sio jambo jema kuwaza kitu ambacho anajua wazi kuwa kitamgharimu maishani.
Muda kidogo akainuka na kuelekea chumbani.
Akaiona simu ya Sam kitandani na kuichukua, akaiangalia na kukuta kuna simu ambazo hazikupokelewa kama tano, hapo akagundua kuwa Sam amesahau simu yake ndiomana imekuwa vile.
Sabrina akaichukua ile simu ili kuangalia kuwa nani aliyekuwa akipiga, ila kabla hajabonyeza ile simu ikaanza kuita tena na namba ilitokea bila jina, Sabrina akaipokea ile simu ila kabla ya kusema 'halow' yule mtu kwenye simu akaanza kuongea na ilikuwa ni sauti ya kike,
"Nilikuwa najaribisha namba yako, mambo vipi lakini? Nipo hapa nje ya nyumba yako."
"Wee nani?"
"Mi nani? Kwani na wewe nani? Mpe mwenye simu wee vipi!"
"Mwenye simu katoka, na mimi ni mke wake sema unataka nini?"
Ule upande wa pili ukacheka,
"Mke wake? Acha kunichekesha dada, toka lini Sam ameoa? Hebu acha kuniletea miujiza, hebu mpelekee simu bhana"
"Kheee mbona unachekesha wee dada, ndio kujifanya unamfahamu Sam sana au? Na kama ungekuwa unamfahamu basi ingekuwa rahisi kwako kutambua kama Sam kaoa. Mimi ni mke wake na nimezaa nae watoto wawili, tena uwe na adabu siku nyingine"
Kisha Sabrina akaikata ile simu na kumfanya alalamike peke yake huku akimshangaa huyu dada,
"Yani ndiomana Sam anawamaliza kiurahisi, wajinga sana hawa. Mtu unamwambia kabisa kuwa mimi ni mkewe ila bado anang'ang'ania"
Ile simu ikaanza kuita tena kwa namba ile ile, Sabrina akaipokea tena,
"Wee dada mi najua kama Sam anamsichana wa kazi ila sio mke kwahiyo kumfanyia kazi Sam kusikufanye ujiite mke umesikia wee malaya eeh! Na umwambie Sam nipo hapa nje ya geti namsubiria"
"Sikia wee dada na unisikilize kwa makini, kama nyumba ya Sam unaijua sana basi ingia. Nini kumsubiria  getini kwani mlango huuoni? Si uingie kama wewe unaijua sana hii nyumba"
"Hebu njoo unifungulie geti wee malaya niingize gari yangu"
Sabrina hakumjibu ila akamsonya yule mwanamke na kuikata ile simu halafu akaizima kabisa na kukaa chini akiongea mwenyewe,
"Hivi huyu Sam huyu ananitakia nini mimi? Kwanini anilete kwenye nyumba ambayo kuna wanawake zake wanakujaga jamani? Yani na kufunga kote ndoa kule bado kuna watu hawajui kuwa Sam kaoa? Ila ngoja huyo mwanamke agonge hilo geti nitamkomesha"
Sabrina alitulia ila hakusikia mtu yeyote akigonga na kuamua kwenda kuchungulia nje ila hakuona kabisa uwepo wa mtu yeyote na kuamua kurudi ndani.

Jeff alipopiga tena simu ya Sam na kukuta haipatikani akazidi kupatwa na mashaka kuwa lazima kuna mabalaa yatakuwa yamewapata tu na kujikuta akikosa raha zaidi na kuamua kwenda kwakina Sabrina ili ajaribu kumueleza alichokikuta na vile ambavyo hawapokei simu na sasa  hawapatikani kabisa.
Alimkuta mama Sabrina akiwa na mjukuu wake mtoto wa James ila James na mkewe hawakuwepo yani walishaondoka.
Jeff akamueleza alichokutana nacho kwenye nyumba ya Sam,
"Kwahiyo wewe ndio ukakimbia sasa?"
"Mama hali ni mbaya kwakweli, nisingeweza kubaki eneo lile. Niliogopa sana"
"Na kweli hiyo hali inatisha, ila Jeff kwahiyo sasa nimekuwa mama yako na sio bibi tena eeh!"
"Aah ni bibi, nisamehe tafadhari. Akili yangu haipo sawa"
"Basi hakuna tatizo, ushasema ile nyumba inamatatizo kwasasa cha msingi tuendelee tu kutafuta mawasiliano yao kwani hata tukisema tuende sijui kama itasaidia. Au ngoja"
Mama Sabrina akafikiria kidogo na kugundua kuwa ana namba ya mlinzi wa Sam na kuamua kuipiga namba hiyo.
Ila alipoipokea tu akawaambia kuwa hawapo kule,
"Sasa watakuwa wapi jamani?"
"Sijui labda wameenda hotelini maana bosi anapenda sana kwenda hotelini"
Ikabidi wakubaliane hivyo na waamini hivyo tu.
Jeff alikubali kwa shingo upande tu kisha akaaga na kurudi nyumbani kwao kwani giza nalo lilishaingia.

Sam aliporudi nyumbani kwake akamshangaa Sabrina kwani hakuna na furaha kama aliyokuwa nayo mwanzoni.
"Vipi tena Sabrina kuna tatizo?"
Sabrina hakutaka kueleza kwani alikuwa na hasira muda huo.
Sam alitambua kama Sabrina alikuwa na hasira ingawa hakujua hasira hizo zimesababishwa na kitu gani kwa muda huo.
Sam akatoa mfuko mdogo mweusi na kumpa Sabrina,
"Chukua hiyo ni zawadi yako"
Sabrina alichukua na kumshukuru Sam ingawa bado hakuwa na furaha.
"Ifungue uone, mbona umeishika tu? Ifungue uonge kuna nini"
Sabrina akafungua na kukutana na simu nzuri mpya na ya kisasa.
"Nimeamua nikuletee simu ili usikae bila mawasiliano"
Sabrina akatabasamu sasa, kisha Sam akainuka na kuelekea zake chumbani kulala.
Sabrina aliiangalia ile simu mara mbili mbili na kuona kuwa kweli Sam kajirudi kwasasa.
Ila alitulia pale sebleni kwa muda sana huku akifurahia ile simu na huku akiogopa kwenda kulala chumbani na Sam kwani alikuwa akijiuliza
"Hivi kwa mfano Sam akinigeuka na kutaka kulala na mimi? Inamaana na mimi ndio itakuwa mwisho wangu kama wale wengine? Na watoto wangu je hawa nitawaacha na nani? Hapana ngoja nilale chumba kingine, ila kama Sam alikuwa na nia mbaya na mimi si angeshanifanyia tangu zamani! Mmh ila naogopa"
Akainuka na watoto wake na kwenda kulala nao chumba kingine.
Aliwalaza watoto na yeye akalala pembeni yao huku akitafakari kuhusu ile simu na akatamani sana kumpigia mtu, kwavile ilikuwa na vocha kwahiyo swala la kupiga halikuwa gumu kwake.
Ila akaona ni vyema aanze kupiga kesho yake ila kila alipojigeuza swala la kupigia simu mtu muhimu sana maishani mwake lilimjia kichwani, na mtu huyo alikuwa ni Jeff.
Akaamua kuichukua simu na kuandika namba ya Jeff kwani namba yake ilikuwa kichwani kisha akaipiga na kuanza kuisikilizia.

Jeff akiwa amekaa chumbani kwake na mawazo sana, akashtuliwa na mlio wa simu na kushangaa kuona ni namba mpya na kumfanya ajiulize kuwa ni nani aliyempigia usiku ule.
Jeff akapotea ile simu na kusikia sauti ya Sabrina,
"Khee Sabrina, Sam yuko wapi?"
"Kalala"
"Huogopi kunipigia usiku? Na je huogopi kulala nae karibu?"
"Kwahiyo hujapenda nilivyokupigia?"
"Hapana sio hivyo Sabrina, tena nimewatafuta toka mchana na hata muda huu nilikuwa sijalala sababu ya kukuwaza wewe na watoto. Mko wapi kwani?"
"Sam katuleta kwenye nyumba yake mpya"
"Afadhari maana nilikuwa na mawazo sana. Nakupenda jamani Sabrina"
Sabrina akakaa kimya kidogo kwani hili neno kila alipoambiwa na Jeff alijikuta akisisimka sana yani tofauti na akiambiwa na Sam.
Wakati Jeff akimsikilizia Sabrina aongee mara akasikia sauti ya kiume ikiita Sabrina na sauti hiyo ilikuwa ya Sam, na muda huo huo simu  ikakatika na kujua wazi kuwa Sabrina amekata simu ile baada ya Sam kumshtukia akiongea nayo.

Sabrina alikata ile simu kwa haraka sana baada ya kusikia sauti ya Sam akimuita, na muda huo huo Sam akafungua mlango wa kile chumba na kuingia ndani. Swali la kwanza alilomuuliza,
"Mbona umekuja kulala huku badala ya kuja kulala chumbani kule na watoto"
Sabrina hakuwa na jibu zaidi ya kumtazama Sam tu,
"Usiwe unaniogopa Sabrina, hivi utaniogopa hadi lini? Na kama ningekuwa na lengo la kukudhuru mbona ningefanya hivyo zamani sana? Ila kwavile watoto washalala basi lala nao tu ila kipindi kingine uwe unajiuliza kwanza kama unachofanya ni sahihi kabla ya kukifanya. Haya sasa kukupa simu imekuwa tatizo, usiku ulikuwa unaongea na nani?"
Sabrina bado alikuwa kimya kwani hata hakuelewa aseme nini ukizingatia ni kweli kafanya makosa.
Sam akamuangalia Sabrina na kusema tena,
"Ndiomana wanawake mnapigwa, na mkipigwa mnadai kuwa mnaonewa ila kwakweli ni makosa yenu. Mimi leo sitasema sana acha nikalale tu"
Sam akatoka na kwenda kulala, Sabrina nae akaweka simu pembeni na kulala sasa kwani hakuamini kama Sam angemuachia tu ukizingatia anajua wazi kuwa ni nani aliyempigia simu kwani alihisi kuwa lazima Sam amesikiliza kidogo mazungumzo yao.

Kulipokucha Sam alikuwa wa kwanza kuamka na kumfata Sabrina chumbani kwake, baada ya salamu tu akamuuliza
"Sabrina, simu yangu iko wapi?"
Sabrina akanywea kidogo kisha na yeye akamuuliza Sam kwa upole sana,
"Ile uliyoniletea jana?"
"Hapana, hiyo ni yako sio yangu bhana na kama nikikuuliza kuhusu hiyo basi nitakuuliza kuwa simu yako iko wapi na sio simu yangu"
"Sawa, simu ipi unayoiulizia sasa?"
"Naulizia simu yangu niliyoiacha jana chumbani nilipoondoka"
Sabrina akakumbuka kuwa hiyo simu alipoizima aliiweka sebleni na kuamua kwenda kuichukua kisha akamuomba msamaha Sam kwa kuizima simu hiyo.
"Na kwanini uliizima sasa?"
Sabrina ikabidi tu aeleze kuhusu mdada aliyepiga simu jana na jinsi walivyojibishana,
"Nisamehe Sam tafadhari"
"Sio tatizo hilo, itakuwa alikuwa anazungumzia nyumba ya kule. Sabrina, hakuna mtu anayepafahamu hapa hata ndugu zangu hakuna ila nitawaleta tu na wewe ukiwa hapa hapa. Ila ngoja niende kule kwangu nikamuangalie Omary kwanza na nione uwezekano wa kumleta huku"
Sam alitoka na kupanda kwenye gari yake kisha akaondoka.
Sabrina alitulia ila alijua wazi kuwa lazima Sam ataenda kumtafuta yule dada wa jana ingawa hakumjua ni nani.

Sam akiwa anaelekea nyumbani kwake akaona kuwa ni vyema ampigie pia huyo dada aliyeongea na Sabrina jana ila simu iliita bila ya kupokelewa akahisi kuwa amechukia kwa kitendo cha kuzimiwa simu.
Ikabidi aendelee tu na safari yake hadi nyumbani kwake na kumkuta mlinzi wake akiwa pale nje kama kawaida.
Sam akasalimiana nae na cha kwanza  kabisa ni kumuuliza kuhusu mdada aliyempigia simu Sabrina kama alikuwa hapo,
"Mmh kwakweli sijamuona bosi, kuna muda nilizunguka nyuma labda ndio alikuja muda huo"
"Haya na hii gari hapa nje ni ya nani?"
"Hata sijui bosi, toka jana ipo hapo hapo. Nadhani ilikuja muda niliozunguka nyuma"
"Ila wewe Omary hujielewi jamani, sijui unafikiri kazi yako ni nini hapa"
"Nisamehe kaka"
"Haya fungua geti niingie"
Mlinzi akatoa funguo ila alivyosukuma geti akashangaa kuwa lipo wazi na kujiuliza kuwa ilikuwaje hadi akasahau kulifunga geti hilo.
Ikabidi tu waingie ndani ya geti hivyo hivyo kabla ya Sam kuanza kumgombeza tena.
Walipoingia walishangaa kumuona mwanamke akiwa chini chali na damu zikimtoka huku mkoba wake na vitu vingine vikiwa hovyo hovyo.
Sam alipomuangalia vizuri yule mwanamke aliona kabisa kuwa ni mwanamke anayemfahamu.

Itaendelea

JE HAYA NI MAPENZI!! 113:

Sam alipomuangalia vizuri yule mwanamke aliona kabisa kuwa ni mwanamke anayemfahamu.
"Kheee Mungu wangu, huyu mwanamke amefikaje humu? Omary amefikaje huyu?"
"Hata mimi sijui bosi"
"Unaumuhimu gani wewe wa kuendelea kuwa hapa wakati kila kitu hujui? Tunafanyaje sasa? Si nilikwambia kuwa asiingie mtu humu ndani jamani!"
Mlinzi hakuwa na cha kujitetea na kumfanya awe kimya tu kwani kila kilichotokea alishangaa kuwa kilitokeaje na ndipo akakumbuka kile kitendo cha kumuona Jeff akitoka mule ndani huku akikimbia na hata alipomuuliza alikimbia zaidi na ni hapo alipoamua kumwambia Sam kuhusu Jeff,
"Kwahiyo hukumpata kumuuliza?"
"Alikimbia bosi, yani alikimbia utafikiri kaona kitu gani"
Sam akafikiria kidogo cha kufanya na jinsi ya kuweza kumsaidia yule dada aliyeanguka pale kwahiyo akawa anajiuliza kama ampeleke hospitali au ampeleke kwa mganga,
"Hata sijui nielekee nae wapi kwakweli, eti nimpeleke kwa mganga au hospitali?"
"Mmh! Huu ni ushirikina bosi kwahiyo hata ukimpeleka hospitali ni kazi bure tu."
"Kwahiyo unashauri twende kwa mganga?"
"Ndio bosi"
"Unadhani kuna atakayenielewa wakati nimeshammaliza mwenzao? Ila ngoja najua cha kufanya, haya mambo yatakuwa sawa tu"
Sam akampita yule mwanamke pale chini na kwenda kufungua mlango wa ndani kisha akaingia ndani kabisa, mlinzi alibaki pale nje akishangaa tu kwani hakuelewa ni kitu gani kinamfanya Sam ajiamini kiasi kile kwani alionekana kutokuwa na uoga wowote na akajiuliza ni vipi ameweze kumuua yule mganga mashuhuri halafu yeye hajadhurika? Na vipi yale mambo ya ajabu yote yaliyotokea pale kwake ila bado anapata ujasiri wa kuingia ndani peke yake? Yule mlinzi aliwaza sana kwani hata yeye tu kwenda kumsogelea yule mwanamke pale chini hakuweza.

Ilipita kama nusu saa Sam akiwa bado ndani na kumfanya mlinzi wake apatwe na mashaka zaidi ila muda kidogo alimuona Sam akitoka ndani na akamuona yule dada akiinuka pale chini na kuwa kama akijishangaa hivi.
Sam alienda moja kwa moja kwa huyu dada na kumwambia,
"Pole sana Janeth"
Yule dada akamtazama Sam na kumkumbatia, ila alipoinuka na kumtazama yule mlinzi wa Sam ilikuwa bado kidogo aanguke tena,
"Vipi Janeth, huyu ni mtu wa kawaida tu"
"Ila ndio nilimkuta hapa chini akitokwa na damu"
Mlinzi wa Sam akashtuka na kuuliza na yeye tena kwa mshangao,
"Ulinikuta mimi nipo chini natokwa damu? Jamani mbona makubwa haya!"
"Ndio nilikukuta wewe na nilipokufata chini ukanikaba na sikumbuki kilichoendelea hadi sasa"
"Wee mdada utakuwa umechanganyikiwa sio bure, sisi tumekushangaa wewe hapa ulikuwa chini unatokwa na damu halafu saivi imekuwa ni mimi loh"
"Ni wewe ndio na nguo zako hizo hizo"
Sam akaona pale mlolongo utakuwa mrefu sana na kuamua kuokota mkoba wa huyu dada kisha kutoka naye nje.
"Kwahiyo na hii ndio gari ulilokuja nalo?"
"Ndio Sam ila nikapatwa na mabalaa"
Akafikiria kidogo na kuuliza,
"Halafu huku nilikuja jioni mbona saa hizi ni kama bado asubuhi?"
Sam hakutaka kumuelewesha kwa muda huo zaidi ya kumsaidia kupanda kwenye gari tu.
Kisha akamwambia yule mlinzi wake,
"Nitamtuma dereva aje achukue hii gari ya nje, ila tafadhari usimruhusu mtu yoyote kuingia hapo kwa kipindi hiki"
"Sawa bosi nimekuelewa"
Sam akapanda kwenye gari ya yule mdada kisha wakaanza safari ya kuelekea nyumbani kwa yule mdada.

Jeff alikuwa na furaha sana siku ya leo ukizingatia kuwa hata ile asubuhi Sabrina alimpigia simu na kumuhakikishia kuwa wapo salama kabisa huku akitamani kwenda kuwaona ila Sabrina alikaa kumuelekeza kwani alihofia pale endapo Sam atagundua swala hili kwahiyo yeye swala la kuwasiliana nae tu lilikuwa ni kheri kwake kwahiyo wakakubaliana kwenda siku atakayopelekwa na Sam.
Muda huu Jeff alikuwa chumbani kwake tu akitafakari hatma yake na Sabrina, ndipo alipopigiwa simu na Aisha.
"Mambo Jeff"
"Poa tu, mbona asubuhi asubuhi"
"Nimekumiss Jeff, huwezi amini ila usiku nimekuota"
"Sawa basi tutaongea badae"
Jeff akakata ile simu kwani hakutaka kuweka mazoea ya karibu sana na Aisha kwani aliona dalili zake hazipo sawa kabisa.
Akaenda zake kuoga na kutoka pale ndani kwao kwa kumuaga mama yake,
"Haya, mi siku hizi sikuulizi maana ushakuwa mtu mzima"
Jeff akacheka tu na kuondoka zake.

Sam alienda hadi nyumbani kwa yule dada,
"Hapa ndipo nilipofikia Sam"
"Kwanza umerudi lini Janeth?"
"Nimerudi juzi"
Kisha akafikiria kidogo na kumuuliza Sam,
"Kumbe Sam umeoa!"
"Nimeoa? Nani kakwambia huo upuuzi?"
"Mmh jamani!"
Kisha akamsimulia majibu aliyopewa jana alipopiga simu.
"Huyo mtu mzushi bhana, mi wala sijaoa."
"Yani nikabaki na mshangao kuwa Sam umenisaliti kweli! Sasa nimeamini kuwa bado unanipenda"
"Ndio Janeth, nakupenda sana. Vipi mzigo umefika nao salama?"
"Tena zaidi ya salama, kwani nimefika na mzigo wote safari hii"
"Wow, ubilionea huo"
Sam akamkumbatia huyu dada kwa furaha.
"Tena leo usiondoke humu, nataka unipe kile ulichoniahidi kwa kipindi kirefu"
"Kipi hicho Janeth?"
Huyu dada akasogea na kuwa kamavile anamnong'oneza Sam,
"Penzi lako"
Hilo neno lilimsisimua sana Sam ila hakutaka kufanya ubaya kwa siku hiyo,
"Kwanini tusifanye siku nyingine Janeth wangu?"
"Mimi nataka leo, yani tusipofanya kwakweli sitakupa ule mzigo"
Sam akafikiria kwa muda kidogo kuhusu swala hilo na kuona wazi kuwa huo mzigo ni wa muhimu sana kwake kuliko maisha ya huyu dada.
"Hilo sio tatizo Janeth, mi wala sitaondoka humu. Nionyeshe basi huo mzigo wenyewe"
Janeth akainuka na Sam kwenda kumuonyesha huko alipoficha mzigo huo.
"Kheee kweli wewe Janeth ni khatari, yani umeweza kuficha mzigo wote huo?"
"Ndio, yani nilikuwa natumia akili sana katika kusafirisha mzigo huo Sam, huwezi amini kwa akili niliyotumia hapo ndiomana nimekawia kurudi."
"Hadi mie nilikata tamaa kuwa utarudi Janeth nikahesabia kuwa nimepata hasara tu ila umefanikisha Janeth. Nashukuru sana"
Wakafurahi sana kwa pamoja kisha wakarudi walipokaa mwanzo  "Na hapa unapoishi ni kwa nani?"
"Nimekodi hapa, nimelipia pesa kiasi kwani najua bosi wangu upo utalipa tu sina shaka kwa hilo"
Sam akatabasamu tu na kusema,
"Hakuna tatizo, nitalipa tu Janeth hata usijali"
"Ile pesa uliyonitumia kipindi kile ndio nikanunulia hiyo gari"
"Hapo ulifanya jambo la akili sana na nitakupa na gari nyingine"
Janeth akafurahi sana na kusahau yote yaliyomkuta nyumbani kwa Sam kisha akainuka na kwenda kuoga kwanza.

Sabrina akiwa pale nyumbani akasikia honi ya gari, moja kwa moja akajua ni Sam amerudi.
Akaenda kufungua geti na gari ikaingizwa ndani na ilikuwa gari ambayo Sam aliondoka nayo asubuhi.
Ila gari iliposimama, aliyeshuka hakuwa Sam bali alikuwa ni kijana mmoja ambaye alishuka na kumsalimia Sabrina kwanza ila kabla Sabrina hajaitikia ile salamu akaulizia kwanza alipo Sam,
"Kwani Sam yuko wapi?"
"Sijui mama, mi alinipigia tu simu kuwa nikachukue gari yake kule nyumbani kwake na kunielekeza niilete huku"
"Mmh makubwa haya, sawa basi nashukuru"
Yule kijana akaondoka zake na kumuacha Sabrina akijiuliza kuwa Sam kaenda wapi na kujiambia kuwa huenda ameamua kwenda na gari nyingine.
Alirudi tu ndani na kucheza na wanae huku akibonyeza bonyeza simu yake.
Akajiwa na kumbukumbu ya namba ya Francis na kuamua kumpigia ila ile simu ilipokelewa na mdada,
"Samahani, namuomba mwenye simu"
"Mwenye simu mimi ni mkewe kwahiyo unaweza ukaniachia maagizo yake"
"Kumbe Francis kaoa?"
"Ndio, ulitaka kumnyemelea? Kaoa na tuna mtoto tayari, kaa huko usitake kunivunjia ndoa"
"Mmh sikuwa na  maana mbaya dada, akija mwambia Sabrina nilimpigia nimsalimie"
Kisha Sabrina akakata ile simu na kujiona kuwa hata yeye anamakosa kumfokea yule mdada wa jana aliposhangaa kuwa Sam kaoa,
"Inawezekana nae alikuwa kama mimi kutokujua kuwa Francis kaoa ingawa Fredy alishawahi kuniambia kuwa Francis ana mwanamke. Ila yule dada wa jana nae hakuwa na kauli nzuri kwangu"
Akakumbuka siku ya kwanza kukutana na Francis kwani alikuwa ndio mwanaume wa kwanza kuvutiwa nae na alikuwa wa kwanza kumfanya ayaone mapenzi machungu.
Akamtafakari sana kisha akaendelea na shughuli zake zingine.

Sam nae hakuwa na ujanja wa kuondoka zaidi ya kumsubiria huyo Janeth, na alipotoka tu bafuni akaenda moja kwa moja alipo Sam huku kajifunga khanga yake tu yenye maji maji.
Sam akaona isiwe shida na akaona ni vyema amalizane nae tu kisha akawatafute wadada wengine ili atimize lengo lake.
Janeth nae alijikoki haswaa akitaka kufaidi penzi la Sam, ila Sam bado alikuwa anasita,
"Kwanini unanifanyia hivyo Sam jamani? Kwanini hutaki kunipa mimi?"
Janeth aliongea hayo kwa sauti ya hamasa na huku akimsogelea Sam na kuanza manjonjo yake ili kumvutia zaidi na kweli Sam naye akavutia, na pale mambo yalipokuwa sawa Sam alimuomba Janeth ageuke ili atimize lengo lake na alipogeuka tu alipiga kelele zisizokuwa na kifani kisha akazimia ila Sam hakumuachia hadi alipomaliza haja yake ndio akamuweka vizuri sasa huku akimuhurumia kuwa ataenda na maji.
Alivaa vizuri nguo zake na kumfunika vizuri Janeth huku akimpa pole.
Kisha akamuinua na kwenda kumpeleka chumbani na kumlaza kitandani kwani hakutaka kumzindua kwa muda huo kwanza mpaka abebe mzigo wake.
Akakaa pale na kumpigia simu kijana wake mkubwa wa biashara hiyo na akamuelekeza pale.
Yule kijana alipofika akapewa ule mzigo na kama kawaida akapeleka sehemu husika wanapotunzia malighafi zao hizo.

Alipoondoka yule mtu sasa ndipo Sam alipoenda na glasi ya maji na kummwagia mwagia Janeth ili azinduke, naye akazinduka na kukaa pale kitandani na kujishangaa kidogo, kumbukumbu nazo zikamrejea huku akisikilizia maumivu makali ya sehemu za siri na kujikuta akilia tu.
"Unenifanya nini Sam? Mbona umenifanyia kitu kibaya sana jamani"
"Nisamehe Janeth, sikutaka kukufanyia hivyo ila ni wewe mwenyewe umelazimisha nikufanyie hivyo. Tafadhari nisamehe sana"
"Umenifanyia dhambi Sam, hapa penyewe nimekufa halafu wewe unaniua tena jamani kwanini umenifanyia hivi? Umenitumia kwa biashara zako na nimefanya bila kinyongo yani fadhila zake ndio kifo?"
"Hapana Janeth, usimwambie mtu nitahakikisha unapona"
"Napona nini wakati umeniongezea tatizo juu ya tatizo, mimi hapa nilipo ni muathirika"
"Kheee ni muathirika? Kwahiyo umenipa mimi ukimwi?"
"Ndio lakini hata hivyo wewe umeniumiza"
Sam akachukia kusikia kuwa yule dada ameathirika na kujikuta akiongea kwa hasira,
"Kwahiyo lengo lako lilikuwa ni kunimaliza mimi kwa ukimwi Janeth? Haya nashukuru kwa ukimwi ulionipa ila huu nitakufa taratibu tofauti na wewe"
Kisha Sam akainuka na kuondoka kabisa.
Janeth akabaki peke yake huku akiugulia maumivu yale.

Sam aliamua kuchukua gari ya kukodi ambayo ilimpeleka moja kwa moja kwenye nyumba yake ya awali kisha akashuka na kama kawaida yule mlinzi wake alikuwepo pale pale getini.
"Haya niambie kuna mauza uza mengine yaliyotokea wakati sipo?"
"Hakuna bosi"
Kisha Sam akaingia ndani na kutoka na gari yake nyingine, halafu akamwambia tena mlinzi wake.
"Narudia tena, usimruhusu mtu yeyote kuingia humu ndani. Sawa?"
"Sawa bosi"
Sam akaondoka huku akili yake ikicheza na idadi ya wasichana ambao anataka kukutana nao kwa siku hiyo ili kuondokana na lile tatizo lililopo kwenye nyumba yake.
"Natakiwa kukutana na wadada watano, Janeth kashawafungulia njia wenzie. Nilitaka kupuuza jambo hili ila huyu Janeth kaniudhi leo na kwavile ameanzisha sina budi kumalizia. Kwahiyo yeye tayari, bado wanne sasa."
Moja kwa moja akaenda baa ya kwanza na kubahatika kumshawishi muhudumu kwa pesa yake kwahiyo akaondoka nae na kwenda nae hotelini huko akamuachia maumivu kama aliyoyapata Janeth kisha akampa pesa na kumwambia asiseme.
Sam alitoka hapo na kumuacha yule dada akilia tu kisha yeye akaenda kwenye baa nyingine ili akutane na mwingine, na alipomaliza hapo akaenda nyingine kwa lengo lile lile huku akijiambia kuwa,
"Mchezo kama huu niliufanya miaka hiyo iliyopita, hatimaye leo imejirudia. Kwakweli lazima nitimize lengo langu"
Kwahiyo akafanya njia ile ile ya kushawishi wadada kwa pesa.

Sabrina alitulia nyumbani bila ya kupata mawasiliano yoyote toka kwa Sam, hadi giza linaingia hakutafutwa na Sam na kuamua ampigie simu,
"Ila Sam unachonifanyia sio sawa kabisa, yani wewe toka umeondoka asubuhi kweli hadi muda huu hata kunipigia simu jamani! Uko wapi sasa?"
"Usijali, narudi sasa hivi"
Kisha Sam akakata ile simu, na muda huo alikuwa ametoka kumliza mdada mwingine hotelini, na kuamua kurudi nyumbani kwake baada ya simu toka kwa Sabrina.

Sam alifika nyumbani kwake na kuingia ndani, akasalimiana na Sabrina pale kisha kuingia chumbani kwake ila kabla hajafanya chochote akakumbuka kuwa katika ile idadi ya wanawake watano kwa siku hiyo amekutana na wanne tu yani bado mmoja na kama akipitiliza siku basi kesho ataanza upya tena idadi itakuwa mara mbili ya siku ya leo.
Akawaza kuwa afanyaje sasa na wakati kasharudi nyumbani, akili nyingine ikamwambia kuwa kwanini huyo mmoja asimalize kwa Sabrina.
Hapo Sam akaamua kumuita Sabrina chumbani.

Itaendelea

JE HAYA NI MAPENZI!! 114:

Akawaza kuwa afanyaje sasa na wakati kasharudi nyumbani, akili nyingine ikamwambia kuwa kwanini huyo mmoja asimalize kwa Sabrina.
Hapo Sam akaamua kumuita Sabrina chumbani.
Sabrina aliyekuwa akimaliza kuwaandaa watoto wake ili walale vizuri, akaamua kuitii ile sauti ya Sam iliyomuita na kuinuka ili aende ila huyu mtoto mdogo akawa analia akaamua kumuweka begani na kwenda nae.
Alimkuta Sam amekaa kitandani ambapo swali la kwanza aliloulizwa Sabrina lilikuwa ni kuhusu mtoto,
"Huyo bado hajalala mpaka muda huu?"
"Ni leo tu ndio kachelewa kulala"
"Haya, niambie na leo utalala chumba gani?"
"Kule naona kumekaa vizuri zaidi"
"Kwahiyo na mimi nije kulala huko?"
Sabrina hapo akakaa kimya bila ya jibu, kisha Sam akamuuliza tena,
"Nini maana ya mke Sabrina?"
"Mke ni mwanamke aliyeolewa na anakuwepo kwa dhumuni la kumsaidia mumewe kwa kila kitu kama kupika, kufua, kuosha vyombo na  mengineyo"
"Bado hujajibu swali langu Sabrina, ni kwanini mwanaume anaamua kuwa na mke ndani?"
"Ili amsaidie hizo kazi"
"Ngoja nikuulize tena, inamaana mwanaume akiwa mwenyewe hatoweza kupika? Kufua na kuosha vyombo? Au mwanaume hawezi kumuajiri mtu kwaajili ya kufanya kazi hizo hadi aoe? Je maana ya kuolewa ni kwenda kumpikia mume, kuosha vyombo na kufua tu? Nini maana ya ndoa? Kwanini watu wanaamua kufanya hivyo?"
Moja kwa moja Sabrina akatambua kile ambacho kinamaanishwa na Sam kwa wakati huo na kujikuta hata akishindwa kumjibu kwani alijua wazi kuwa ni kigumu kwake.
"Mbona kimya tena Sabrina? Wewe ni mke wangu si ndio?"
Sabrina akaitikia kwa kutikisa kichwa, Sam akainuka na kumsogelea Sabrina kisha akamshika bega na kumwambia,
"Hata mchungaji siku ya ndoa alikiri kuwa hawa si wawili tena bali wamekuwa mwili mmoja. Sabrina unatakiwa kunipa haki yangu kama mume wako tena wa ndoa kabisa"
Sabrina aliinama na machozi yakamtoka na kumuangukia mtoto aliyekuwa amembeba ambapo Sam akamsogelea karibu na kumkumbatia, kisha akamwambia
"Kamlaze mtoto Sabrina unipe haki yangu"
Ni hapa ambapo Sabrina akaamini kuwa Sam anamaanisha kile anachokisema ukizingatia alikuwa akisisitiza kabisa.

Sabrina alitoka mule chumbani na mwanae huku akielekea chumba kingine, alimuangalia mwanae aliyekuwa akilia bado na kumuweka pembeni kisha na yeye kukaa kitandani na kujikuta akitokwa na machozi mfululizo.
Moyo wake ulibeba mzigo ukubwa sana wa maumivu huku akiwahurumia watoto wake na kujua wazi yale aliyokuwa anasema kwamba wanawake wanaponzwa na tamaa basi na yeye ameangukia kwenye kundi hilo la wenye tamaa kwani kama angebaki kwao basi yasingemkuta hayo ukizingatia anaujua ukweli wote kuhusu Sam ila kingine akawaza kuwa kama angebaki kwao bado ingekuwa ni ngumu sana kwake kujieleza kwa mama yake.
Sabrina alilia sana bila ya  kujua cha kufanya kwa wakati huo, na mtoto wake naye alikuwa akilia hata yule aliyemlaza sebleni yani Cherry naye aliamka na kuanza kulia.

Sam alitoka hadi sebleni na kumkuta Cherry akilia ambapo Cherry alipomuona Sam alishuka pale kwenye kiti na kumfata Sam ili ambebe ambapo Sam alimnyanyua mtoto yule na kumuweka begani.
Siku zote Sam alikuwa na upendo sana kwa huyu mtoto Cherry, alijikuta akimpenda kama mwanae wa kumzaa kabisa na kile kilio chake cha kutoka usingizini ndicho kilichomsononesha na kumfanya ambebe huku akimbembeleza.
Akajikuta pia akisikia sauti ya kilio cha yule mtoto mdogo wa Sabrina ila haikumuumiza kama sauti ya Cherry ilivyomuumiza.
Akiwa amembeba Cherry begani, Sam akaenda nae chumbani alipo Sabrina na kumkuta akiwa kajiinamia akilia.
Sam akamtua Cherry kwenye mikono ya Sabrina na kumwambia,
"Mpende sana huyu mtoto"
Kisha akawaacha pale na kutoka, na aliondoka kabisa kwa muda huo kwani Sabrina alisikia tu mlio wa gari ya Sam likitoka.

Sabrina akajifuta machozi sasa na kuanza kuwabembeleza watoto kwanza kwani wote wawili walikuwa wakilia.
Alimuangalia sana Cherry na kutokuelewa kuwa kwanini Sam anampenda sana mtoto huyo kwani alihisi kuwa ndio aliyemsaidia kusamehewa na adhabu ya Sam.
Ingawa ilikuwa ni usiku, Sabrina hakutaka hata kufikiria alipoenda Sam kwani alichofikiria kwa muda huo ilikuwa ni kuhusu yeye na watoto wake tu. Akili ya haraka haraka ikamjia kuwa atoroke pale nyumbani kwa Sam huku akijiwazia kuwa ataondokaje kwa usiku huo? Akaona jambo rahisi ni kuwasiliana na Jeff na kumuelekeza hata maeneo ya yeye alipo ila tatizo lilikuwa kwamba lile eneo bado mgeni kwahiyo hakulijua vizuri na kumfanya kufikiria hata uwezekano wa kupata labda gari ya kukodi.
Vyote vilikuwa ni vigumu kwake na kumfanya aone vyema kupiga simu kwa Jeff tu na muda huo huo akachukua simu yake na kumpigia Jeff,
"Nina matatizo Jeff "
"Matatizo gani tena?"
"Naomba tuonane halafu nitakueleza tatizo langu"
"Tuonane muda huu Sabrina? Tuonane wapi?"
"Ngoja nitakwambia, subiri nipate gari ya kukodi"
Kisha Sabrina akakata ile simu.
Akawaandaa watoto wake, mmoja akambeba mgongoni na mwingine akamshika mikononi kisha akaanza kuondoka.
Alipofika mlangoni ili afungue mlango akashangaa ni mgumu, alipoujaribisha tena akagundua umefungwa kwa nje,
"Sam kanifungia mlango nadhani alikuwa na wazo langu kabla yangu"
Ikabidi arudi na kukaa kisha akaona vyema kuwa bora aende chumbani tu kulala na watoto kwani hapakuwa na namna nyingine.

Jeff alikuwa na mshangao tu na kubaki na maswali kuwa Sabrina kapatwa na nini kwa wakati huo ila alitulia kwa muda bila ya Sabrina kupiga simu tena wala kusema kinachoendelea kwa wakati huo, hivyobasi akaamua kumpigia simu yeye mwenyewe ili amuulize vizuri,
"Sabrina mbona kimya  tena, kwani tatizo ni nini?"
"Tatizo ni Sam kafunga mlango"
"Kivipi? Kwani Sam yuko wapi?"
"Sijui alipo ila usijali, nikipata nafasi tu nitakueleza kilichotokea"
"Kwanini usinieleze sasa hivi Sabrina? Nieleze tu, kwani kuna tatizo gani?"
Sabrina aliamua kumueleza Jeff kwa kifupi kile kilichotokea,
"Unaona sasa Sabrina mama angu, huko unajitafutia makubwa tu yani. Huyo Sam si mtu mzuri na anaweza kukugeuka na wewe kama alivyowageuka hao. Ingawa sijui chochote kuhusu Sam ila ile barua ya Neema ilijieleza kila kitu"
"Usitaje jina hilo Jeff"
"Jina gani? Neema au?"
"Ndio hilo hilo usilitaje, ile nyumba ya mwanzo balaa zote zililetwa kwa jina hilo"
"Haya tuachane na yote hayo halafu tuangalie cha kufanya sasa baada ya hayo yaliyotokea"
"Sijui cha kufanya, nishauri chochote tu Jeff"
"Mmh ningekuwa napajua huko ingekuwa rahisi, ila ngoja na mimi nifikirie cha kufanya"
"Sasa itakuwaje? Naangamia mwenzio huku ujue"
Mara akasikia muungurumo wa gari na kujua kwa vyovyote vile Sam amerudi tayari na kujikuta akikata simu kwa uoga akihofia kumkera zaidi.

Sam aliingia ndani kwake na moja kwa moja akaenda chumbani kwake kulala huku akifikiria alichokifanya muda mfupi uliopita na yote aliyoyafanya kwa siku hiyo.
"Ni kweli nimefanikisha malengo yangu ila hiki nilichokifanya mwishoni sijakipenda kwakweli. Sam mimi nitakuwa na dhambi ngapi? Ni wangapi wamelia sababu yangu? Ni wangapi wameteseka, kwanini nimekuwa hivi mimi?"
Alijisikitikia ila ndio tayari alishatenda matendo ambayo hayafai kabisa katika jamii.
Sam alijifikiria sana na bado kile kitendo alichokifanya mwishoni kilisumbua akili yangu na kumfanya asikitike sana kwani huwa hapendi kuwaumiza mabinti wadogo na kwa siku hiyo ndio alichokifanya katika harakati zake za kuhakikisha kuwa anatimiza kile alichoamriwa.
Sam hakuweza kulala kabisa sababu ya mawazo na   kumfanya aamue kuchukua vinywaji vyake vikali na kunywa ili tu kutuliza mawazo.

Jeff akajaribu tena kupiga namba ya Sabrina ila haikupokelewa kwavile Sabrina alishamweleza kuhusu kilichotaka kumpata akajikuta akiwa na hofu juu ya hilo na jambo la haraka kwake kwa wakati huo aliona ni bora aende tena kule kwa Sam kwa zamani akamuulize yule mlinzi ingawa alishakutwa na majanga ila alijipa moyo hivyo hivyo kuwa lazima akapate jibu ukizingatia tayari ameshajua kuwa ile nyumba ina matatizo gani.
Kwahiyo Jeff akaamua kutoka nyumbani kwao na kumuaga mama yake,
"Jamani Jeff usiku huu!"
"Kuna vitu naenda kushughulikia mama"
"Hata kama sio kwa usiku huu Jeff"
"Mama, mimi ni kijana mkubwa sasa na nina mishe nyingi tu ndiomana kuna kipindi nilikwambia kuwa nikapange ila ukasisitiza niendelee kuishi hapa basi niachie uhuru mama yangu. Najielewa na ninatambua ninachokifanya mama. Usiwe na mashaka yoyote juu yangu"
Sakina hakuw na neno zaidi ya kumruhusu tu mwanae afanye anachotaka, kisha Jeff akatoka na kuondoka.

Jeff alienda hadi stendi ila kwa muda ule ilikuwa ngumu kidogo kupata usafiri wa daladala hivyobasi akaamua kusogea kwa madereva wa bodaboda na kukodi moja wapo ili imfikishe mahali angalau apate daladala, lakini walipokuwa njiani wakamuona dada mmoja akiwa amekaa pembezoni mwa barabara huku akilia.
Huruma ikamshika Jeff na kumfanya amuombe yule dereva wa bodaboda asimamishe ili aweze kumuhoji maswali yule dada ila dereva wa bodaboda alionekana kuwa na harakati za kuwahi abiria wengine,
"Utaniongezea pesa kaka"
"Ila mbona nyie mpo hivyo jamani yani unajali pesa kuliko utu!"
"Nipo kutafuta pesa hadi usiku huu na kama ningejali utu basi ingekuwa nimelala muda huu"
"Basi nitakuongezea hiyo pesa"
Jeff akashuka na kumfuata yule dada, alipommulika na mwanga wa simu yake alimuona wazi kuwa yule dada bado ni mdogo sana hata akamshangaa kwa usiku ule,
"Umekumbwa na nini binti?"
Huyu dada alilia tu na alishindwa kujibu, Jeff akamuomba ainuke nae ili aende nae kwao.
Ila yule binti alipoinuka, sketi yake ilionekana kulowa damu na kumfanya Jeff aulize tena
"Kwani umetoa mimba"
"Hapana"
Huyu binti alijibu huku akilia.
Jeff akamuomba mwenye bodaboda ili wapande pamoja na yule binti,
"Itabidi uniongezee hela tena maana haturuhusiwi kupandisha mishikaki"
"Nimekwambia hakuna shida nitakuongezea tu"
Jeff akapanda na yule binti kisha wakaanza safari ya kurudi kwao na kusahau kabisa kilichomtoa kwao kwa usiku ule ni nini kwani alijikuwa na huruma iliyopitiliza dhidi ya yule binti.

Sabrina alikuwa ndani katulia kabisa akiogopa hata kupokea simu aliyokuwa anapigiwa na Jeff kwani alijua wazi kama Sam akimsikia basi ataamua kufanya kitu chochote kile hata kama ameghairi kwahiyo kwa wakati huo akaona ni vyema alale kabisa na kuzima simu yake kabisa.

Jeff alifika nyumbani kwao na kushuka na yule binti, akamlipa pesa dereva wa bodaboda kisha yeye na yule binti kuelekea ndani kwao ambao Jeff aligonga kwanza mlango na mama yake kwenda kufungua.
Sakina akamshangaa Jeff akiwa ameambatana na yule binti,
"Vipi tena jamani?"
"Nimemkuta huyu binti njiani mama, anaonekana kuwa na shida nikaamua kumsaidia"
Kwa jinsi yule binti alivyokuwa ikambidi Sakina atoe khanga yake na kumfunika kisha kumuongoza bafuni akaoge na aweze kuwaeleza vizuri.
Alipomaliza kuoga, Jeff akapendekeza waongee nae kesho kwani ni usiku sana na wangemuacha apumzike tu ambapo Sakina aliafiki hilo na kumpeleka chumba cha kulala wageni ili apate kupumzika kwa usiku huo kisha Jeff nae akaenda chumbani kwake na alipojaribu kuipiga simu ya Sabrina haikupatikana tena ila akaona ni vyema swala la Sabrina ashughulike nalo pia kesho yake,
"Najua kama Sabrina kapatwa na tatizo basi atatokea msamalia mwema wa kumsaidia kama mimi nilivyomsaidia binti huyu."
Kisha akaamua kulala tu.

Kulipokucha kwa upande wa Sabrina, aliamka na watoto wake kama kawaida na alipotoka sebleni alimkuta Sam yupo pale sebleni amekaa tu.
Sabrina akamsalimia ila Sam hakuitikia na kumfanya Sabrina ahisi kwamba kaamua kumchunia tu.
Kisha akawakalisha wanae na kwenda kuwaandalia chakula, akarudi na kuwalisha ila bado Sam alikuwa kakaa vile vile na kumfanya Sabrina apatwe na uoga kidogo kwani si kawaida ya Sam kabisa.
Sabrina alipomalizana na wanae akaamua kumfata tena Sam pale kwenye kiti ili amuulize kilichomsibu,
"Sam mbona upo kimya sana?"
Sam hakujibu, na kumfanya Sabrina ajaribu kama kumuinua kichwa Sam alimshangaa akiwa ametoa tu macho na wala hayazunguki.
Sabrina uoga ukamjaa zaidi, na alipomuachilia kile kichwa akashangaa akianguka kwenye kochi.

Itaendelea

JE HAYA NI MAPENZI!! 115:

Sam hakujibu na kumfanya Sabrina ajaribu kama kumuinua kichwa Sam alimshangaa akiwa ametoa tu macho na wala hayazunguki.
Sabrina uoga ukamjaa zaidi, na alipomuachilia kile kichwa akashangaa akianguka kwenye kochi.
Kitendo kile bado kidogo kimfanye Sabrina akimbie kwani mule ndani watu wenye utambuzi wao ni wawili tu yani yeye na Sam halafu Sam ndio huyo kapatwa na tatizo, hakujua afanye nini na kuona akili yake ikichanganyikiwa kwani Sam alikuwa kamavile mtu aliyekufa kabisa.
Sabrina alikaa pembeni akijiinamia kwani hakujua kitu cha kufanya kwa muda huo.
Wakati Sabrina akiwa amejiinamia, yule mtoto wao Cherry aliinuka alipo na moja kwa moja akaenda alipo Sam na kumfanya Sabrina atake kumkataza kwani alimuona akiinuka na kuelekea kwa Sam ila roho nyingine ilimwambia amuache ili aone kuwa yule mtoto anaenda kufanya kitu gani.
Cherry alipomfikia Sam, akawa kama anamgusa usoni ila mikono yake ikaelekea kwenye pua ya Sam na gafla Sam akainuka na kupiga chafya kama mara tatu kisha akamtazama Cherry na kutabasamu ambapo Cherry nae alikuwa akitabasamu kisha Sam akamnyanyua mtoto yule na kumuweka miguuni mwake.
Sabrina alikuwa akishangaa tu hiki anachokiona kwa muda huu kwani hakukielewa kabisa ila Sam alionekana kawaida kamavile hakuna kitu chochote kilichotokea kwake.
Ni hapa sasa Sabrina alipoamua kuvunja ukimya na kuuliza,
"Sam una tatizo gani?"
"Tatizo? Kivipi?"
"Unajua hali niliyokukuta nayo haikuwa ya kawaida kabisa ila hapo unaonekana upo kawaida tatizo ni nini?"
"Kwani umenikuta na hali gani?"
Ikabidi Sabrina amueleze alivyokuwa na jinsi Cherry alivyomsogelea, ila cha kumshangaza Sabrina ni kuwa Sam hakuzungumzia ile hali bali alifurahia kitendo cha Cherry tu,
"Ooh wow, ndiomana nakapenda haka katoto jamani. Badae nitamletea zawadi yake, mtoto ana akili sana huyu ndiomana nikampa hili jina"
Sam alikuwa na furaha tu kisha akainuka na kumuweka Cherry halafu yeye akaenda chumbani kwake na kumfanya Sabrina abaki na maswali tu bila majibu yoyote yale.

Kwa upande wakina Jeff ilikuwa tofauti kidogo kwani iliwabidi wawahi kuamka kutokana na sauti ya kilio iliyotoka kwa yule binti wa usiku.
Sakina aliona ni vyema wamuhoji huyo binti kisha wampeleke kwa mjumbe kwavile kulishaanza kupambazuka tayari.
"Kwani binti unaitwa nani?"
"Naitwa Amina"
"Nini kimekupata? Kuwa wazi ili iwe rahisi kwetu kukusaidia"
"Ona damu zinavyonitoka na sehemu za siri zinaniuma nalia kwa uchungu ila nimeambiwa nisiseme"
"Usiwe muoga binti, napenda kujua tatizo ni nini na kwanini upo hivyo ili nijue jinsi ya kukusaidia"
Sakina alikuwa akimbembeleza binti huyu ili aongee kinachomsibu, Jeff nae alikuwa pembeni akisikiliza kwa makini kwani huruma yake kwa yule binti ilikuwa ya hali ya juu.
Sakina aliendelea  kumbembeleza yule binti ili aseme ukweli wa kilichomsibu,
"Amina, hata usiwe na mashaka sisi tunataka useme ukweli halafu tujue tunaanzia wapi kukusaidia"
"Ni hivi jamani, mimi nilikuwa na wenzangu tulienda disko yani kwa mara ya kwanza katika maisha yangu kwenda disko hata nyumbani hawajui kama nilienda huko. Wakati tumetoka disko tukajikuta hatuna pesa kabisa ya kuweza kupata usafiri wa kurudi nyumbani ndipo wenzangu wakatoa ushauri kuwa tuombe lifti. Tukakubaliana hilo na kwenda barabarani kusimamisha gari za kuomba lifti cha kushangaza tulipofika barabarani kuna gari ikaja wenzangu wakapanda na kuniacha peke yangu nilishtukia tu hawapo hapo ndio nikachanganyikiwa zaidi kuona Asha na Rose wameniacha mwenyewe ikabidi nami nisimamishe gari kweli likasimama na nikamuomba lifti akakubali ila wakati nipo kwenye gari yake alinirubuni na kuniingila kimwili....."
Hapo alinyamaza na kuangua kilio tena,
" Jamani pole sana binti yani alikubaka?"
"Ndio, na bora kama angekuwa mwanaume wa kawaida ila alikuwa ni jini"
Na kulia tena, Sakina akashikwa na huruma pia kwa huyu binti kwani siku ya kwanza kufanya makosa ndio siku hiyo hiyo akakutana na mabalaa.
"Pole sana, kwahiyo hakuwa mtu alikuwa ni jini! Mungu wangu, ulijuaje sasa kama ni jini?"
"Alipokuwa ananiingilia, maumbile yake yalibadilika na kuwa na miba yani bila huruma akaniingilia hivyo hivyo"
Sasa Amina alizidisha kilio zaidi tena kilikuwa kilio cha kwikwi hata Sakina nae machozi yakamtoka kwani aliweza kuhisi ni maumivu gani yule binti kayapata  alipokuwa anaingiliwa kimwili na huyo mtu, alijikuta akimuhurumia sana kwani kwa yale maelezo tu hata yeye mwenyewe alihisi kuumia.
Yule binti aliendelea kuelezea huku akilia,
"Nililia sana na kupiga makelele ila hakunionea huruma kwakweli yani hakunionea huruma kabisa. Na alipomaliza akapeleka gari yake  mbele na kunishusha kisha akaniambia kuwa usimwambie mtu yoyote na kunitupia pesa chini kisha akaondoka. Muda ule ule nikiwa nalia wakatokea vijana wawili vibaka na kunipora kila kitu na kuniacha pale nikilia. Sijui mimi nitawaeleza nini wazazi wangu jamani"
Amina alikuwa akilia tu, Sakina akamsogelea karibu kama kumbembeleza na kumlaza kifuani mwake kwani alikuwa akilia sana ila gafla waliona kimya na hakutoa sauti yoyote wakajua kuwa amenyamaza sasa,
"Pole sana Amina"
Jeff nae akaongea kwa masikitiko,
"Inaumiza sana hii hacri jamani ila atapona tu Mungu atamsaidia jamani"
"Na bora kanyamaza sasa"
Kisha Sakina akamuangalia yule binti pale kifuani pake na kumwambia,
"Usijali binti, mimi nitakutetea kwa wazazi wako. Kwani wanaishi wapi?"
Sakina akashangaa kimya yani yule binti hajibu tena na wala halii tena,
"Vipi amelala au"
"Hata sijui"
Kisha Sakina akawa anamuweka pembeni kwa kumuita, ila alivyokuwa anamuweka akashangaa kumuona kalegea kabisa yani wala hatingishiki tena,
"Mungu wangu, nini hiki?"
Sakina aliinama na kusikiliza mapigo ya moyo ya yule binti ila hakuyasikia na kumfanya agundue kuwa yule binti hapumui tena.
Sakina akajikuta akirukia pembeni,
"Inamaana amekufa?"
"Nini mama amekufa?"
"Ndio, hebu muangalie kwanza"
Sakina alihisi kuchanganyikiwa sasa, Jeff aliinama na kumsikilizia yule binti naye akagundua kuwa amekufa,
"Khee mama tutafanyaje sasa?"
"Kwakweli sijui tutafanyaje maana hapa nilipo hata akili imenipotea"
Walijikuta wakimuangalia mara mbili mbili yule binti bila ya kujua wafanye nini.

Sam alipotoka chumbani kwake akamwambia Sabrina,
"Sitaki utoke humu ndani ndiomana unaona kuwa nilikwambia kama kuna msichana wa kazi atakuwa anakuja ila hujamuona hadi leo kwavile nimemsitisha kwa muda. Najua hapo ulipo unamawazo ya kutoroka ila usiwe na wazo hilo ukiwa na mimi"
Sabrina alikuwa kimya akimsikiliza tu Sam kwa anachoongea,
"Jana nilitingwa na ndiomana nikafikia hatua ile Sabrina ila kwakweli mimi siwezi kukufanyia chochote kibaya yani siwezi kabisa ila jana nimefanya dhambi sana"
Hapa ndio Sabrina akauliza kuwa ni dhambi gani ambayo Sam anaiongelea,
"Kwani umefanya dhambi gani Sam?"
"Ngoja nikwambie ukweli Sabrina ingawa bado sijakumalizia historia kuhusu mimi na kwanini nimefikia hatua ya kufunga ndoa na wewe"
Sam akakaa kimya kidogo na kuwa kama mtu anayefikiria jambo ambapo wakati huo Sabrina nae alitulia kabisa akimsikiliza Sam.
"Niambie basi huo ukweli"
"Jana nilipatwa na matatizo Sabrina, unajua yule mzee kule nyumbani kwangu bado ananisumbua"
"Mzee gani?"
"Yule mganga au umemsahau?"
"Namkumbuka, si ulisema kuwa unaenda kumaliza kiburi cha yule mzee wewe!"
"Ndio nilimaliza kiburi chake"
"Ulikimalizaje sasa na jana amekusumbuaje?"
"Yule mzee nilimuua na ....."
Sabrina akashtushwa sana na hii kauli ya Sam kuwa alimuua yule mzee tena alimshangaa Sam kwa kuongea vile tena kwa ujasiri kabisa,
"Sasa mbona unashtuka? Inambna hujawahi kusikia mtu kauwawa au ni vipi?"
"Hapana nimeshangaa tu kwani sikujua kama tatizo ungelimaliza kwa kumuua yule mzee kwahiyo ulimuua vipi?"
"Kwani wengine wanaua vipi? Mi nilimpiga risasi tu na ukawa mwisho wa habari yake"
Sabrina alibaki kutoa macho tu kwani aliweza kugundua kuwa Sam ni katili kwa kiasi gani ila hakutaka kujionyesha mshtuko wake kwa kuhofia kugeukiwa na yeye.
"Sasa ndio umemuua jana?"
"Sijamuua jana, ni siku kadhaa zimepita tangu nimuue ila cha kushangaza kuna matukio ya ajabu sana yanatokea pale nyumbani"
Sam akamueleza Sabrina kuhusu tukio la yule dada kutokwa na damu, na yale maelezo ya Sam yakamfanya Sabrina aelewe moja kwa moja kuwa huyo mwanamke ndio huyo aliyebishana nae majuzi yake na kumwambia aingie ndani.
Kwahiyo Sabrina alikuwa ametoa macho tu akimsikiliza Sam na yale maelezo yake, ambapo Sam aliendelea kuelezea kwa alichokifanya jana sasa,
"Niliona hali itazidi kuwa mbaya ukizingatia nataka kuuza ile nyumba, ikabidi niingie ndani kwanza ili nikaongee na malaika wangu"
Hapo napo Sabrina akashangaa ila akaona kama akionyesha mshangao wake basi Sam anaweza akasimama kumsimulia kuhusu hilo tukio kwahiyo akatulia kumsikiliza Sam,
"Malaika wangu akaniambia kuwa natakiwa nitoe kafara ya wadada watano na kafara hiyo inatakiwa nilale na hao wadada ila wewe uliponipigia simu na kufanya nirudi ilikuwa bado mdada mmoja na kama nisingefanikisha jana basi ningetakiwa leo kuanza upya tena mara mbili ya jana. Kwahiyo nisamehe sana kuhusu jana"
"Kwahiyo jana ulitaka kunitoa kafara na mimi?"
"Nisingeweza fanya hivyo kwa mapenzi niliyonayo kwa Cherry, umeona na leo alivyoweza kunirudisha? Huyu mtoto ni baraka sana katika maisha yangu na ninakuapia leo kuwa lazima nimletee zawadi"
Sabrina bado alikuwa na swali kuhusu huyo malaika anayeongelewa na Sam kwani bado hakuelewa kabisa, ni hapo alipoamua kumuuliza Sam,
"Na huyo malaika ni nani?"
"Kwani hujui malaika? Ni jini anayenilinda, yule niliyepewa kipindi kile nilipokuwa na nia ya kuwakomesha wanawake. Huwa siwezi zungumza naye wakati kuna mtu ndiomana huwa naingia mahali peke yangu"
Sabrina alizidi kushangazwa tu na maelezo ya Sam kwani bado yalimshtua na kumfanya azidi kumuona Sam ni mtu wa ajabu kwa kila neno kwani swala la kuongea na jini kwa binadamu wa kawaida halikuwa swala la kawaida.
Kisha Sam akamueleza kwa kifupi kile alichokifanya usiku,
"Nilipoondoka hapa nilikuwa nawaza mwanamke wa kwenya kumalizana nae na mawazo yangu yakalenga moja kwa moja kwa wadada wanaojiuza ila kwa bahati mbaya au nzuri nikamkuta mdada njiani aliyesimamisha gari yangu nami nikampakiz a kwenye gari kisha kumalizana nae ila kile kitendo kinaniumiza hadi muda huu"
"Kwanini kile kitendo kinakuumiza?"
"Jua tu kinaniumiza, ila ngoja nikalete zawadi ya Cherry. Hoja ni ile ile sitaki utoke nje Sabrina"
Kisha Sam akainuka na kutoka kabisa, ule mlango akaufunga kwa nje kama alichokifanya usiku.
Sabrina alibaki akitafakari tu yale maelezo ya Sam.

Baada ya Sam kuondoka Sabrina bado hakuelewa kuwa Sam ni mtu wa aina gani na kama anaweza kuutoa uhai wa mtu yeyote bila ya uoga, vipi kwa uhai wake sasa. Kwakweli Sabrina alijiona yupo kwenye moto ambao unachochewa kila kukicha bila ya yeye kujua.
Ni hapa alipoamua kwenda kuichukua simu yake na kujaribu kumpigia simu Jeff ili aweze kumueleza kwa kifupi tu, ila ile simu iliita sana bila ya kupokelewa na kumfanya Sabrina ajiulize kuwa Jeff anatatizo gani na kwanini hapokei simu yake.
Kisha akaona ni vyema kuwasiliana na kwao pia ili asalimiane na mama yake kwa muda huo.

Jeff na Sakina bado hawakujielewa cha kufanya na yule Amina kwani kwa upande wao ilikuwa ni mtihani mkubwa sana ukizingatia yule alikuwa marehemu tayari na hata ndugu zake hawawafahamu.
"Tutafanyaje sasa jamani!"
"Mama, tumpeleke tu hospitali maana hakuna namna nyingine"
"Ujue ni kesi hii Jeff! Hali ni mbaya mwanangu sijui hata mimi jamani"
Mara wakasikia mtu akigonga mlango na kuwafanya washtuke wote wawili ila yule mtu alipoona hakuna majibu aliamua kuingia ndani mwenyewe kwavile mlango haukufungwa na funguo, akawakuta Jeff na mama yake wakimshangaa tu kwani hawakutegemea ujio wake, na huyu alikuwa ni baba wa Jeff. Naye aliwashangaa pia,
"Vipi nyie hamkutegemea kuniona!"
Walikuwa kimya tu, kisha huyu baba akaangalia chini na kushangaa, halafu akawauliza
"Huyu mwanangu Amina amefika vipi huku?"
Jeff akashtuka pia kusikia kuwa Amina ni mtoto wa baba yake kwahiyo ni ndugu yake.

Itaendelea







USISAHAU KU LIKE PAGE YETU,BONYEZA LIKE BUTTON

No comments:

Theme images by pollux. Powered by Blogger.