*MBINU NA SIRI YA KUFANIKIWA KIUCHUMI MAISHANI MWAKO*

UTAMU KITANDANI APP
Kwanza kabisa tambua ndoto yako Ni nini au unataka kuwa nani ktk maisha yako.
Panga malengo yako,
Weka mipango ya kufanikisha ndoto yako,
Weka utekelezaji wa mambo uliyopanga,
Simamia mipango yako kikamilifu bila kulegeza wala kupunguza Kasi,
Usiache fursa yoyote ikakupita bila kuifuatilia, hakikisha unaifuatilia hadi mwisho ili ujiridhishe.
Pia penda kusoma vitabu mbalimbali vya kiuchumi, kijasiriamali, mambo ya fedha, pia unaweza kutumia simu yako Kama silaha ya kuufuta umaskini Maishani mwako.
Usipuuze fursa yoyote Ile, pia usisikilize maneno ya watu Wala kuhisi kuwa watakuonaje.
Bali fanya utafiti wa kina kuhusu kina fursa yoyote kabla ya kuifanyia kazi ili ujiridhishe Kama Ni ya kweli au hapana, ukishaona kuwa Ni ya kweli na itakulipa fanya bila kuogopa chochote au mtu yeyote.
Kingine ili ufanikiwe kimaisha, inabidi ujifunze kwa waliofanikiwa siyo walioshindwa.
Maana walioshindwa maisha watakukatisha tamaa kuwa haiwezekani kupata mafanikio ktk kitu fulani unachotaka kufanya wakati huenda yeye alishindwa kwa kufanya fulani au kukiuka kanuni za mafanikio ya jambo hilo bali waliofanikiwa watakupa mbinu za kufanikiwa ktk maisha yao.
Jambo jingine Kama unataka kufanikiwa ktk maisha yako,
jifunze kuwa na msimamo mkali ktk maamuzi yako unayofanya hasa ukishagundua na kujiridhisha kuwa unachotaka kufanya kina manufaa kwako au jamii Wala usikubali mtu au kitu fulani kikuyumbishe ktk maamuzi yako hasa pale unapogundua kuwa jambo unalofanya lina manufaa kwako au kwa jamii yako inayokuzunguka,
maana binadhamu tunafanana kwa nje tu ila kwa kifikra na kimaono pamoja na kimtazamo tunatofautiana sana tena mbali sana.
Focus yako si sawa na ya mwingine, kumbuka kuwa maisha yako Ni dhamana yako.
Hivyo hakuna atakaayekujali au kuyajali maisha yako Kama wewe hauyajali,
Mwisho kabisa uwe mkweli na muwazi kwa watu wako wako unaofanya nao kazi halafu mwombe na kumtdnguliza Mungu ktk kila jambo unalofanya.
Nakuhakikishia kuwa ukifuata kanuni hizo utapepea juu tu Kama tai, nakutakia mapambano na maisha mema yenye mafanikio tele.




USISAHAU KU LIKE PAGE YETU,BONYEZA LIKE BUTTON

No comments:

Theme images by pollux. Powered by Blogger.